Mwagala News

Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Latest Post

Image result for magufuli
Rais  John Magufuli amemteua Prof Andrew Barnabas Pembe kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi kupitia Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa imesema kuwa uteuzi wa Prof. Pembe umeanza siku ya leo.
Kabla ya uteuzi huo Prof. Pembe alikuwa Mhadhiri  na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia taaluma, utafiti na ushauri.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa ahirisho la mwisho katika kesi ya kutumia lugha ya matusi dhidi ya Rais John Magufuli  inayomkabili mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee.
Tokeo la picha la HALIMA MDEE MAHAKAMANI
Akizungumza leo Ijumaa Juni 1, 2018 Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ametoa ahirisho hilo la mwisho kwa upande wa mashtaka baada ya wakili wa Serikali mwandamizi, Patrick Mwita kudai kesi ilipangwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa, hawana shahidi ikiwa ni mara ya tatu.

Baada ya kutolewa maelezo hayo, hakimu Simba alitoa ahirisho la mwisho na kupanga kesi hiyo kusikilizwa tena Juni 29, 2018 kwa mashahidi wa upande wa mashtaka kuanza kutoa ushahidi.

Katika kesi hiyo Mdee anadaiwa kufanya kosa hilo Julai 3, 2017 Makao Makuu ya Chadema yaliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni.

Anadaiwa kutamka “anaongea hovyo hovyo, anatakiwa afungwe breki” kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Halima alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Julai 10, 2017. Katika kesi hiyo mbunge huyo  anatetewa na mawakili, Peter Kibatala, Jeremiah Mtobesya na Hekima Mwasipu.

Benki ya Exim nchini imefanya hafla fupi ya futuru (Iftar) pamoja na wateja wake huku ikibainisha iko katika mchakato kupunguza riba ili kuwawezesha wateja kunufaika na mikopo na huduma nyingine  zitolewazo na benki hiyo.

Hatua hiyo imekuja hivi karibuni baada ya tamko la Serikali kupitia Waziri wa Fedha na Mipanga, Philip Mipango lililoyataka taasisi za kibenki kupunguza riba za mikopo kwa wateja ili waweze kunufaika.
Kaimu Mkurugenzi wa benki ya Exim Bw. Selemani Ponda akiongea na waandishi wa habari mara baada ya futari iliyofanyika hoteli ya New Afrika mapema jana jijini Dar es salaam. 

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Exim, Selemani Ponda wakati wa hafla hiyo iliyowakutanisha wafanyakazi na wateja wa benki hiyo.

Amesema benki hiyo huwa na utaratibu na kukutana na wateja wake katika Kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramdhani na kwamba tayari imeshafanya hivyo katika mikoa mingine ikiwemo Tanga, Mwanza na Mtwara.
“ Tumekutana na wateja wetu katika tafrija fupi ya Iftra mwezi huu wa ramdhan hatufanyi hapa hata mikoa mingine tumeshajumuika na wateja wetu nia ni kuwa nao karibu,” amesema.

Amebainisha kuwa tamko la Serikali la kuzitaka taasisi za kifedha kupunguza riba wamelisikia na mchakato wa kulifanyia unaendelea na kwamba wakati utakapofika riba zitawekwa wazi kwa wateja wao.
Amesisitiza kuwa benki inaamini bado inaendelea kutoa huduma bora kwa wateja wake huku akiongeza kupunguzwa kwa riba ni njia mojawapo ya kuwanufaisha kwa kuwapatia riba nafuu.

Kwa upande wake, mteja wa benki hiyo, Moustafa Khatan ameziomba benki kutoa riba nafuu  na kuajiri wazawa kwa usawa katika nafasi mbalimbali.
Naye Mwanzilishi wa Chama cha Watoa Huduma ya Oil na Gesi nchini(ATOGS) ambaye pia ni mteja wa benki hiyo, Abdulsamad Abdulrahim ameipongeza benki ya Exim kwa kuwakutanisha na kuiomba iendelee kutoa huduma bora.

Iran,US nuclear dealRis wa Iran, Hassan Rouhani, amesema kwamba endapo rais Trump atafanikiwa kusitisha makubaliano ya mpamgo wa nuklia na Tehran, Marekani itambue wazi itakabiliwa na "majuto ya kihistoria"
Tamko hilo la rais Rouhani, lililotolewa kwenye runinga, limekuja wakati waziri wa masuala wa nchi za nje wa Uingereza wa kigeni, Boris Johnson, amekwenda mjini Washington kama sehemu ya jitihada za kumshawishi rais Trump na utawala wake wasiutelekeze mpango wa nyuklia.
Tarehe ya mwisho ya kutoa maamuzi kwa serikali ya Marekani juu ya Iran inatarajiwa kufikia ukingoni wiki moja ijayo.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani alisema rais wa Marekani amesisitiza ahadi yake ya kuhakikisha kwamba Iran haipati kamwe silaha ya nyuklia. Na katika siku za hivi karibuni, Rais Trump alimweleza rais wa Ufaransa aliyekuwa ziarani na viongozi wa Ujerumani kwamba anaamini makubaliano ya kimataifa ya kukabiliana na mpango wa nyuklia wa Iran ulikuwa mzuri sana.
Wakati wote Korea Kaskazini imekuwa ikiikosoa Marekani , lakini kumekuwa na mashambulizi machache katika wiki za hivi karibuni, wakati wa mipango ya Rais Trump kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un.
Taarifa hii ya karibuni ni kama tahadhari ya kuwa majadiliano kati ya nchi hizo mbili hayatakuwa rahisi.Wakati huo huo Korea ya Kaskazini imeishutumu Marekani kwa uchochezi wa makusudi dhidi ya Pyongyang kwa kutoa ushauri wa vikwazo havitaondolewa mpaka hapo itakapondoa silaha zake za nyuklia.
Wakati huo huo Korea ya Kaskazini imeishutumu Marekani kwa uchochezi wa makusudi dhidi ya Pyongyang kwa kutoa ushauri wa vikwazo havitaondolewa mpaka hapo itakapondoa silaha zake za nyuklia.
Wakati wote Korea Kaskazini imekuwa ikiikosoa Marekani , lakini kumekuwa na mashambulizi machache katika wiki za hivi karibuni, wakati wa mipango ya Rais Trump kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un.
Taarifa hii ya karibuni ni kama tahadhari ya kuwa majadiliano kati ya nchi hizo mbili hayatakuwa rahisi.
CHANZO BBC NEWS

Image result for katibu mtendaji baraza la mitihani tanzania
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Dk. Charles Msonde

NA MWANDISHI WETU, DAR

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza kufanika kwa Mitihani ya kidato cha sita na ualimu ambapo itafanyika kuanzia kesho (leo)  7 hadi 25 Mei 2018 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam jana ,  Katibu Mkuu wa Baraza hilo Dokta Charles Msonde alisema kuwa jumla ya watahiniwa 87643 wamesajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha sita mwaka huuu  ambapo kati yao  wa shule ni 77222 na  wa kujitegemea ni 10421.

Dk. Msonde alifafanua kuwa  katika katika kuelekea kufanya mtihani huo, jumla ya Shule za Sekondari zitakazo fanyika mtihani huo ni 674,  vituo vya watahiniwa wa kujitegemea  231 huku vyuo vya ualimu vikiwa 125 kwa Tanzania bara na Zanzibar

Aliongeza kuwa  kati ya watahiniwa wa shule 77222 waliosajiliwa kufanya mtigahi huo , wavulana  ni 45105 sawa na  asilimia 58.41,wasichana  32117 sawa na asilimia 41.59.

Aidha aliongeza kuwa  “ katika  watahiniwa hao,kuna wenye ulemavu waskuona, ambapo wao pia wanahaki ya kufanya mtihani huo, na jula yao kwa mwaka huu wapo 12 na wale  wenye uono hafifu wapo 56 ambapo maandishi ya karatasi zao hukuzwa” alifafanua Dk. Msonde.

Hata hivyo kwa upande wa mtihani wa ualimu jumla ya watahiniwa ni 7422 wamesajiliwa kufanya kozi za ualimu kwa ngazi ya  cheti  na Stashahada ambapo kati yao wavulana  ni 4931 na wasichana  ni 2491.

Dk. Msonde alieleza kuwa , idadi ya watahiniwa waliosajiliwa katika ngazi ya Cheti ni 5234 ambapo wavulana ni 3204 na  wasichana  2030, huku  watahiniwa waliosajiliwa kwa  ngazi ya Stashahada ni 2188 ,wavulana  1727 na  wasichana 464.

 

 Akizungumzia maandalizi ya mtihani huo alisema kuwa  yamekamilika kwa asilimia 100 nchi nzima ikiwa ni pamoja na kusambazwa Mitihani hiyo kwa wahusika, vitabu vya kujibia sambamba na  nyaraka zote muhimu katika mikoa  Tanzania Bara na Zanzibar.

Sambamba na hilo, aliwakumbusha wananchi kuthamini na kutambua umuhimu wa wanafunzi kufanya Mitihani hiyo kwakuwa  ndio daraja la pekee la kufikia mafanikio yao.

"Pia nitumie fursa hii kutoa wito kwa kamati za Mitihani ,Halmashauri,  Manispaa na Majiji yote kuhakikisha kuwa taratibu za Mitihani zote zinazingatiwa,   nawaonya mjiepushe na mianya ya rushwa kwani Baraza hatutasita kuwachukulia hatua stahiki” alisistiza Dk. Msonde.

Aliongeza kuwa “ wito wangu pia kwa wananchi tunaomba ushirikiano katika kipindi hiki, unaruhusiwa kutoa taarifa za kiuhalifu ama uvunjwaji wa sheria za Mitihani na kuripoti sehemu husika. "


Mwishooo.

Ujumbe wa Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete katikati ya wiki hii uliteka mtandao wa kijamii wa Twitter na kusambaa kwenye Whatsapp, akionesha sehemu ya maisha yake baada ya urais.

Dkt. Kikwete ambaye alihamia Msoga mkoani Pwani kwa ajili ya mapumziko baada ya kutoka Ikulu, aliwepa picha kadhaa akiwa anakula chakula kwenye sahani na bakuli moja na wazee ambao walihudhuria msiba wa baba yake mdogo, Said Lumaliza katika kijiji cha Msigi.

“Tukila chakula na ndugu zangu msibani kwa baba yangu mdogo marehemu Said Lumaliza(1917-2018) katika kijiji cha Msigi karibu na Msoga. Hii ndiyo fahari ya maisha ya kustaafu.!” alitweet mara mbili kwa Kiswahili na Kiingereza, Machi 8.

Watumiaji wa mtandao huo ambao wengine walitoka nje ya nchi walisifu maisha ya kujishusha ya rais huyo mstaafu na kueleza kuwa ni viongozi wachache waliokuwa na cheo kama chake ambao wanaweza kurejea kwenye maisha ya aina hiyo.

“Kuna Maisha baada ya kustaafu. Itafika muda ulinzi kamili itakua ni yale uliyo wafanyia watu na ndicho nilicho jifunza hapo,” aliandika Samuel Isaya.

“Wewe ni rais wa mfano kwa Afrika pamoja na kuwa na mapungufu yako kama binadamu. Hongera sana mhe Mungu akutangulie ktk muda wote wa Maisha yako,” Zakayo Sarwatt.

“It’s very rare to see a former African president from any African country spending time with low class citizens,” aliandika Hermescash. Kwa tafsiri isiyo rasmi, “Ni mara chache sana utaona marais wa zamani Afrika kutoka nchi yoyote wakitumia muda wao na watu wa hali ya chini.”

Ikiwa kila tarehe 8 ya mwezi machi nchi zote duniani zinasherekea siku ya mwanamke duniani kwa kufanya mambo mbalimbali ikiwa ni kuenzi na kupongeza michango mbalimbali iliyotolewa ama inayoendelea kutolewa na wanawake.
Mkurugenzi mtendaji wa Lecri Consult Bi. Edna Kamaleki akitoa ufafanuzi wa jambo fulani kwa wageni waalikwa, katika maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani mapema leo jijini Dar es salaam.

Katika kuhakikisha siku hii inaenziwa vyema mashirika mawili yaliyoamau kuungana na kufanya kitu kizuri kwa siku hii nayo ni Lecri Consult pamoja na Hodari Tanzania.

Na kwa mujibu wa kauli mbiu ya kimataifa ya mwaka huu inayosema “Chagiza maendeleo yako” hii ikijaribu kuwapa msukumo wanawake katika kujitafutia maendeleo yao wenyewe.

Mashirika hayo yameenzi siku hii kwa kufanya kongamano na wanawake pamoja na wanaume ili kuwajuza mambo mbalimbali ikiwa  ni haki na wajibu wao kama wanawake na pia kuwapa mwanga wanaume nini cha kufanya ili kupunguza vitendo vya ukatili wa wanawake na watoto.

Katika kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa British Council jijini Dar es salaam liliudhuliwa na maafisa mbalimbali kutoka serikalini na asasi za kiraia ili kuweza kubadilishana uzoefu na kuelimishana mengi kuhusu haki zao kama wanawake.

Lakini pia katika kongamano hilo waliweza kuwaonyesha kwa kiasi gani wanawake wanaweza kuwa wamiliki wa ardhi yao wenyewe kwa mujibu wa sharia na sio kila siku kuwa nyuma ya mwamvuli wa wanume.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Hodari Tanzania Bi. Emelda Lulu Urio akiongea na wageni waalikwa waliohudhuria tafrija ya maadhimisho ya siku ya Mwanamke duniani iliyofanyika British Council jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Hodari Tanzania Bi. Emelda Lulu Urio akiendelea kutoa elimu kwa wanawake na wanaume waliofika katika tafrija hiyo.
Mkurugenzi wa LAPF kanda ya Dar es salaam Bi. Amina Kassim kiwaelezea wageni waalikwa fursa zinazopatikana katika shirika hilo na kwa kiasi gani LAPF inawajali wanawake kwa kuwapa huduma stahiki kwa gharama nafuu.
Mkurugenzi wa LAP kanda ya Dar es salaam Bi. Amina Kassim akiongea na wageni waalikwa.

Afisa Ustawi Jamii wa wilaya ya Ilala Bi. Francisca Makoye akielezea wao kama ustawi wa jamii nini majukumu yao na wanafanya nini ili kuwakomboa wanawake dhidi ya ukatili wanaofanyiwa na wanaume zao au jamii kwa ujumla.

Mkurugenzi wa Benki ya NMB tawi la Samora Bw. Sospeter Magesse akielezea kwa namna gani benki hiyo inafanya kazi kwa ukaribu kwa kushirikiana na wanawake kote nchini.
Maafisa kutoka mashirika mbalimbali ya kiserikali na binafsi wakifuatilia kwa umakini mawasilisho yanayotolewa na wawezeshaji.

Washiriki wa maadhimisho wakiwa katika picha ya pamoja.

    ANGALIA VIDEO HII KUJUA MENGI YALIYOTOKEA..
                     

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget