RUSHWA ni miongoni mwa vitu vinavorudisha nyuma maendeleo ya
nchi nyingi duniani, kutokana na kukwamisha maendeleo na kusababisha kukosekana kwa
haki, utawala bora wa sheria na uvunjifu wa sheria katika nchi nyingi
duniani.
Licha ya kuwa rushwa ni tatizo kwa nchi nyingi duniani, lakini kuna
nchi zinatajwa kuwa na kiwango kidogo cha rushwa huku sababu kubwa
ikitajwa kuwepo kwa utawala bora, uwazi katika kufanya maamuzi na
kiwango kizuri cha maisha.
Kwa mujibu wa Corruption Perception Index hizi ndizo nchi 10 zenye kiwango kidogo cha rushwa kwa mwaka 2017.
1: Denmark
Licha ya kuwa miongoni mwa nchi zenye furaha duniani, Denmark inatajwa pia kuwa nchi namba moja yenye kiwango kidogo cha rushwa ambapo kwa mujibu wa Corruption Perception Index nchi hiyo inapata 92% kwa mwaka 2017.
2: New Zealand
Ni nchi namba mbili kuwa na kiwango kidogo cha rushwa duniani ambapo
sababu kubwa inayofanya nchi hii kuwa na kiwango kidogo cha rushwa ni
uwepo wa utawala bora. Serikali ya New Zealand hufanya maamuzi kwa uwazi na hali nzuri ya kiuchumi. 3: Finland Miongoni mwa sababu inayoifanya Finland
kuwa na kiwango kidogo cha rushwa kwa mujibu wa taasisi ya kuchunguza
rushwa duniani ni uwepo wa hali ya haki na usawa na hali nzuri ya
kiuchumi. Imepata 89%. 4: Sweden Kwa mujibu wa Katiba ya Sweden,
Bunge lina nafasi kubwa ya kufanya maamuzi ukilinganisha na serikali.
Hali hii inaifanya serikali ya nchi hiyo kuogopa kufanya makosa ya
rushwa kwa sababu ya Bunge kuwa na nguvu kubwa. Aidha, katika nchi hii
matumizi mabaya ya madaraka huonekana pia kama rushwa. 5: Norway Norway ni miongoni mwa nchi zenye kiwango kidogo cha rushwa, na kwa mujibu wa Corruption Perception Index, inapata 86% kwa kuweza kupambana na rushwa kwa mwaka 2017. 6: Switzerland Switzerland imefanikiwa
kupambana na rushwa kwa 86% na kwa mujibu wa taasisis ya kupambana na
rushwa, nchi hiyo imefanikiwa kwa sababu Katiba yake inaruhusu wananchi
kujihusisha katika majidiliano wakati serikali inafanya maamuzi kupitia
njia ya kura za maoni. 7: Singapore Kwa mujibu wa Corruption Perception Index, Singapore
imefanikiwa kwa zaidi ya 84% kupambana na rushwa na inatajwa kuwa nchi
ya saba kwa mwaka 2017 kuwa na kiwango kidogo cha rushwa. 8: Uholanzi Uholanzi ni miongoni mwa nchi zinazotajwa na Corruption Perception Index kwa kuwa na kiwango kidogo cha rushwa ambapo sababu kubwa inayochangia ni uwepo wa program za kuzuia rushwa. 9: Luxembourg Inatajwa kuwa moja kati ya nchi ndogo na tajiri zaidi katika nchi za
Umoja wa Ulaya ambapo sababu kubwa inayoifanya nchi hiyo kuwa mongoni
mwa nchi zenye kiwango kidogo cha rushwa ni hali ya uchumi kuwa nzuri
kwa kila raia wa nchi hii. 10: Canada. Canada ni
miongoni mwa nchi zenye kiwango kidogo cha rushwa duniani ambapo moja ya
sababu kubwa inayochangia kuwepo kwa kiwango kidogo cha rushwa ni Bunge
la nchi hiyo kuwa na nguvu zaidi ya serikali hivyo kupelekea serikali
kufanya maamuzi kwa uwazi na utawala bora.
Image caption
Meli ya kubeba ndege za kivita ya USS Carl Vinson (kushoto) na meli nyingine zilielekea Bahari ya Hindi
KUNDI la meli za
kivita za Marekani, ikiwemo meli yenye uwezo wa kubeba ndege za kivita,
hazikuwa zinaelekea upande wa Korea Kaskazini kama ilivyoripotiwa awali,
bali zilikuwa zinaelekea eneo tofauti.
Jeshi la wanamaji la
Marekani lilikuwa limetangaza 8 Aprili kwamba kundi hilo la meli
likiongozwa na meli kubwa ya Carl Vinson lilikuwa likielekea rasi ya
Korea, kama hatua ya kuionya Korea Kaskazini.
Wiki iliyopita, Rais wa Marekani Donald Trump pia alitangaza kwamba kundi kubwa la meli za kivita lilikuwa likitumwa eneo hilo.
Lakini imebainika kwamba ukweli ni kuwa meli hizo zilikuwa zinaelekea eneo tofauti.
Taarifa zinazsema kwamba kufikia mwishoni mwa wiki, zilikuwa zimesafiri mbali sana na
rasi ya Korea na zilikuwa zinapitia mlango wa bahari wa Sunda kuingia
katika Bahari ya Hindi.
Wakuu wa jeshi la wanamaji la Marekani
katika Bahari ya Pasifiki walisema Jumanne kwamba walikuwa wamefutilia
mbali safari ya meli hizo katika bandari ya Perth.
Hata hivyo,
wanajeshi wake walikuwa wamekamilisha mazoezi ya pamoja ya kijeshi
yaliyokuwa yamepangwa awali kati ya majeshi ya Marekani na Australia
katika pwani ya kaskazini magharibi mwa Australia.
Baada ya mazoezi hayo, meli hizo zilielekea Singapore mnamo Aprili 8 mwaka huu, kundi hilo la meli sasa "linaelekea Magharibi mwa Pasiki kama lilivyoamrishwa".
Mwandishi
wa BBC anayeangazia habari za Korea Stephen Evans anasema bado
haijabainika iwapo kulitokea suitafahamu katika mawasiliano au labla
Marekani ilipotosha watu makusudi kujaribu kumtia wasiwasi kiongozi wa
Korea Kaskazini Kim Jong-un.
Awali, Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence
alionekana kutoyumba alipohutubia wanahabari akiwa kwenye meli ya kivita
ya USS Ronald Reagan ambayo imetia nanga Japan.
Aliapa kwamba
Marekani iko tayari "kushinda shambulio lolote na kukabiliana na
matumizi yoyote ya silaha za kawaida au za nyuklia kwa nguvu zake zote."
Korea
Kaskazini na Marekani zimekuwa zikijibizana vikali viki za hivi
karibuni na safari ya meli hizo ilikuwa imeibua uwezekano wa Marekani
kutekeleza shambulio la mapema kujaribu kulemaza mfumo wa kijeshi wa
Korea Kaskazini.
Jumatano, Pence alitaja taifa hilo kuwa
"tishio kubwa zaidi na la dharura kwa amani na usalama" katika maeneo ya
Asia na Pasifiki. Chanzo BBC NEWS