Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Latest Post

Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi akielezea jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa taasisi hiyo Profesa Godwin Mjema na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala toka wizara hiyo Bw. Stephen Mushi.
PIX2
Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT), Profesa Godwin Mjema akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala toka wizara hiyo Bw. Stephen Mushi.
PIX3
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Bi. Segolena Francis akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam.
PIX4
Mtaalamu wa Utafiti kutoka Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT),akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa  taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
PIX5
Baadhi ya washiriki wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) wakiwa katika kikundi cha majadiliano hayo yaliyofanyika  leo Jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo limewashirikisha wadau wa sekta ya ujenzi kutoka sehemu mbalimbali.
PIX6
Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi (wanne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya ujenzi mara baada ya kufungua kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam.
Picha na Idara ya Habari (MAELEZO)
……………………….
Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inatarajia kuanzisha Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) ili kuweza kuzalisha wataalam wa ngazi ya kati wenye ubobezi katika sekta ya ujenzi.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Barabara Mhandisi John Ngowi wakati wa kongamano la pili la kujadili hatua mbalimbali zilizofikiwa juu ya uanzishwaji wa Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Mhandisi Ngowi amesema kuwa kuanzishwa kwa taasisi hiyo hapa nchini kutawezesha kuondoa pengo la uwiano baina ya wahandisi na kada za chini kama mafundi sanifu na mafundi mchundo ambao ndio wasimamizi wa karibu wakati kazi za ujenzi zinapotekelezwa.
“Mpango mkakati wa Wizara yetu pamoja na mambo mengine, unahusisha uimarishwaji wa sera zinazohusu ujenzi kwa kujenga mazingira wezeshi,mafunzo ya ufundi na matumizi ya teknolojia mkakati ambao utawezesha kutatua changamoto za umahiri na ubobezi inayokabili sekta ya ujenzi,” amesisitiza Mhandisi Ngowi.
Aidha, Mhandisi Ngowi ameongeza kuwa  uanzishwaji wa taasisi hiyo itakuwa chachu ya kufikia azma ya serikali ya awamu ya tano katika kuelekea uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025 kwa kuongeza rasilimali watu ambao ni muhimu katika usanifu, usimamizi, ujenzi na ukarabati wa miundombinu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ni mshauri wa uanzishwaji wa ICoT  Profesa Godwin Mjema amesema kuwa mipango ya  uanzishwaji wake umefikia hatua nzuri ambapo umeshirikisha wadau mbalimbali ili kujadili Kozi na mitaala itakayotumika kufundishia.
“Sisi kazi yetu ni kushauri na leo tumekutana na wadau kujadili hatua tuliyofikia, wadu watajadili na kukubaliana na yale tuliyoandaa, wakikubaliana na sisi tutakabidhi kwa wizara ambao ndio wamiliki na wao watawasilisha Baraza la Taifa Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa hatua za usajili,”. amesema Profesa Mjema.
Kuanzishwa kwa taasisi hii kunatokana na kuendelea kupanuka kwa pengo kati ya waandisi na kada za chini hali iliyotokana na vyuo vingi vya ufundi kupandishwa hadhi kuwa vyuo vikuu katika miaka ya 1990 bila kuanzishwa vyuo vingine vya ngazi ya kati hasa vya fani ya ujenzi.
Imetolewa na kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano.

Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi akielezea jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa taasisi hiyo Profesa Godwin Mjema na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala toka wizara hiyo Bw. Stephen Mushi.
PIX2
Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT), Profesa Godwin Mjema akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala toka wizara hiyo Bw. Stephen Mushi.
PIX3
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Bi. Segolena Francis akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam.
PIX4
Mtaalamu wa Utafiti kutoka Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT),akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa  taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
PIX5
Baadhi ya washiriki wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) wakiwa katika kikundi cha majadiliano hayo yaliyofanyika  leo Jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo limewashirikisha wadau wa sekta ya ujenzi kutoka sehemu mbalimbali.
PIX6
Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi (wanne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya ujenzi mara baada ya kufungua kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam.
Picha na Idara ya Habari (MAELEZO)
……………………….
Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inatarajia kuanzisha Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) ili kuweza kuzalisha wataalam wa ngazi ya kati wenye ubobezi katika sekta ya ujenzi.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Barabara Mhandisi John Ngowi wakati wa kongamano la pili la kujadili hatua mbalimbali zilizofikiwa juu ya uanzishwaji wa Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Mhandisi Ngowi amesema kuwa kuanzishwa kwa taasisi hiyo hapa nchini kutawezesha kuondoa pengo la uwiano baina ya wahandisi na kada za chini kama mafundi sanifu na mafundi mchundo ambao ndio wasimamizi wa karibu wakati kazi za ujenzi zinapotekelezwa.
“Mpango mkakati wa Wizara yetu pamoja na mambo mengine, unahusisha uimarishwaji wa sera zinazohusu ujenzi kwa kujenga mazingira wezeshi,mafunzo ya ufundi na matumizi ya teknolojia mkakati ambao utawezesha kutatua changamoto za umahiri na ubobezi inayokabili sekta ya ujenzi,” amesisitiza Mhandisi Ngowi.
Aidha, Mhandisi Ngowi ameongeza kuwa  uanzishwaji wa taasisi hiyo itakuwa chachu ya kufikia azma ya serikali ya awamu ya tano katika kuelekea uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025 kwa kuongeza rasilimali watu ambao ni muhimu katika usanifu, usimamizi, ujenzi na ukarabati wa miundombinu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ni mshauri wa uanzishwaji wa ICoT  Profesa Godwin Mjema amesema kuwa mipango ya  uanzishwaji wake umefikia hatua nzuri ambapo umeshirikisha wadau mbalimbali ili kujadili Kozi na mitaala itakayotumika kufundishia.
“Sisi kazi yetu ni kushauri na leo tumekutana na wadau kujadili hatua tuliyofikia, wadu watajadili na kukubaliana na yale tuliyoandaa, wakikubaliana na sisi tutakabidhi kwa wizara ambao ndio wamiliki na wao watawasilisha Baraza la Taifa Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa hatua za usajili,”. amesema Profesa Mjema.
Kuanzishwa kwa taasisi hii kunatokana na kuendelea kupanuka kwa pengo kati ya waandisi na kada za chini hali iliyotokana na vyuo vingi vya ufundi kupandishwa hadhi kuwa vyuo vikuu katika miaka ya 1990 bila kuanzishwa vyuo vingine vya ngazi ya kati hasa vya fani ya ujenzi.
Imetolewa na kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano.

1
United States Embassy Chargé d’Affaires, Dr. Inmi Patterson delivers remarks during the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) at a ceremony in Dodoma.
2
Prime Minister Kassim Majaliwa, United States Embassy Chargé d’Affaires Dr. Inmi Patterson (on his left) and senior Government Ministers officials officiates the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) in Dodoma.
3
United States Agency for International Development (USAID), Mission Director, Andrew Karas (2ndleft) and the Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, Ms. Ummy Mwalimu (right), following the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) at a ceremony in Dodoma.
……………………..
Dodoma (September 5) – Prime Minister of the United Republic of Tanzania, Kassim Majaliwa officiated the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) today at a ceremony in Dodoma. He was joined by U.S. Embassy Chargé d’Affaires Dr. Inmi Patterson and a number of senior Government officials and Ministers, reflecting the wide-reaching impact of PlanRep and FFARS across sectors and government institutions.
Developed in partnership with the U.S. Government through the United States Agency for International Development (USAID), these computer-based information management systems will play complementary roles in preparing plans and budgets and standardizing financial management at every level of government. In particular, these platforms will ensure the efficient, transparent, and accountable use of funds among Local Government Authorities (LGAs) and facilities, paving the way for improved delivery of public services to citizens.
Introduced over a decade ago as a planning, reporting, and budgeting tool for LGAs, PlanRep’s redesign marks a number of improvements over its predecessor. Whereas the original version was accessed offline, with users across the government relying on different versions of the software, the updated system provides a uniform, online format accessible anytime, anywhere. Additionally, the new web-based version allows PlanRep to share documents and information with other government information systems, eliminating the lengthy, error-prone process of uploading documents manually. With over 1,500 users trained to use the new system, PlanRep will operate across all public sectors to provide a more efficient, transparent, and accountable system of providing public services to citizens.
While PlanRep assists with planning, budgeting, and reporting revenue across multiple levels of government, FFARS serves as an accounting and reporting system for facilities such as schools and health centers, where funding for public services is increasingly being managed. FFARS offers service providers a simple, standardized, set of documents and processes that enable them to record the availability and source of their funding for core services at each facility. FFARS also tracks how funds are used and ensures compliance with procurement regulations and reporting requirements. With this information, the Government of Tanzania will maintain a more robust public financial management system that increases transparency so that service providers are more accountable to the communities and organizations they serve.
“The United States is proud to partner with Tanzania as you work toward a future marked by transparent government, sustainable development and shared prosperity,” remarked Chargé d’Affaires Inmi Patterson of the U.S. Embassy in Dar es Salaam during the ceremony. “Together, these two systems will increase efficiency and improve financial management, enabling the Government of Tanzania to more effectively distribute its financial resources and respond to citizen needs.”
U.S. Government support to PlanRep and FFARS falls under the USAID Public Sector Systems Strengthening (PS3) activity. Designed in partnership with the Government of Tanzania, PS3 works in 13 regions and 93 LGAs to strengthen public service delivery through improved governance, finance, human resources, and information systems. In addition to the design and rollout of PlanRep and FFARS, PS3 recently supported the launch of a standardized website layout for regional secretariats and LGAs nationwide earlier in March of this year.
To request more information, please call the U.S. Embassy Dar es Salaam Press Office at Tel: +255 22 229-4000 or email: DPO@state.gov; or The President’s Office – Regional Administration and Local Government (PO-RALG). Tel: +255262320024 or Email: dict.staff@tamisemi.go.tz

1Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akisalimiana na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, ACP Hamisi Issa, mara alipowasili katika mkoa huo akiwa njiani kuelekea mkoa wa Arusha, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo ili kujua changamoto wanazokutananazo wakati wakitekeleza majukumu yao


2Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (kushoto), akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara alipowasili katika mkoa wa Kilimanjaro, akiwa njiani kuelekea mkoa wa Arusha, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo ili kujua changamoto wanazokutananazo wakati wakitekeleza majukumu yao, kulia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, ACP Hamisi Issa.
3Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (kulia), akizungumza na Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ally Lugendo, na Mkuu wa chuo cha Polisi Moshi (CCP), SACP Ramadhan Mungi (kushoto), mara alipowasili katika mkoa wa Kilimanjaro, akiwa njiani kuelekea mkoa wa Arusha, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo ili kujua changamoto wanazokutananazo wakati wakitekeleza majukumu yao.
Picha na Jeshi la Polisi.

Lameck Ditto.

BAADA ya ngoma zake mbili alizotoa hivi karibuni kudaiwa kubuma, staa wa Wimbo wa Moyo Sukuma Damu, Lameck Ditto ‘Ditto’ amefunguka kuwa habari hizo siyo za kweli, kwani kwa upande wake anaona ziko vizuri.

Akichonga na Risasi Vibes, Ditto alisema ngoma zake hizo ambazo ni Bembea na Nabadilika hazijabuma kwani siku zote amekuwa akifanya muziki ambao umekuwa na mashabiki wengi kwa hiyo hauwezi kukwama kwenye vyombo vya habari ‘media’ hata siku moja.

“Nimeona kwenye mitandao ya kijamii watu wakidai nyimbo zangu nilizoachia hivi karibuni zimebuma, hilo si kweli maana kama ni video nimepeleka kwenye media mbalimbali na zinapigwa kwa hiyo watu waache kuzungumza vitu ambavyo havina ukweli ndani yake,” alisema Ditto.

Kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja

Mshambuliaji mpya wa Simba, John Raphael Bocco anatarajiwa kuikosa mechi ya watani wa Jadi 'Ngao ya Jamii' inayochezwa leo jioni katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kutokana na kutokuwa vizuri kiafya.

Hayo yamebainishwa na Kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja wakati alipokuwa anazungumza na mashabiki zao kupitia mtandao wao na kusema wamejiandaa vizuri kuwapa raha mashabiki watakaojitokeza uwanja wa Taifa kutazama mtanange huo kwa kuwa wanakikosi kizuri kilichokamilika.

"Sisi kama Simba tunahitaji ushindi katika mechi ya leo kwa sababu itatusaidia kutuweka katika nafasi nzuri huko mbeleni. Wachezaji wote wako vizuri kasoro wawili ambaye ni John Raphael Bocco pamoja na Said Mohamed. Nawaomba mashabiki wa Simba waje kisimba kisimba kuipa ushirikiano timu yao iwapo uwanjani ili wachezaji waweze kufanya vizuri zaidi ya vile walivyopanga kufanya leo", alisema Mayanja.

Kwa upande wake, Nahodha wa Simba Method Mwanjali amesema wamejipanga vizuri kuelekea mechi hiyo ambayo imekuwa yenye kutazamwa kwa jicho pana na mashabiki wao ili waweze kupata furaha ya ushindi.

Bonyeza Links Zifuatazo Kusoma zaidi na Kuapply

6 Jobs Opportunities at NMB Tanzania

Job Opportunity at Vodacom Tanzania

Job Opportunity at Qatar Airways, Reservation & Ticketing Supervisor

Job Opportunities at Mwananchi Communication Limited

Job Opportunity at Standard Bank, Officer, Credit Risk Management

Job Opportunity at Standard Bank, Officer, Accounts Payable

Job Opportunity at Palladium Group (Tanzania) Limited, Program Manager

Job Opportunity at Sunda Investment Co Limited, Customer Service Supervisor

Nafasi zaidi Ingia www.ajirayako.co.tz


Kiungo mpya wa timu hiyo, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima.

WAKATI kikosi cha Simba leo hii kikishuka uwanjani kupambana na Yanga katika mchezo wa Ngao ya Jamii, kiungo mpya wa timu hiyo, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima ameondolewa kwenye jukumu la kupiga penalti.

Niyonzima ambaye amejiunga na Simba hivi karibuni akitokea Yanga kwa kitita cha Sh milioni 115, huenda asipige penalti kwenye mchezo wa leo, endapo hali hiyo itatokea.

Hali hiyo inatokana na kuonyesha uwezo wa chini wa kupiga penalti katika mazoezi ya juzi jioni na jana asubuhi ya timu hiyo ya kujiandaa na mechi hiyo Ngao ya Jamii yaliyofanyika katika Uwanja wa Boko Veterani uliopo Ununio nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Katika mazoezi hayo, penalti zote alizopiga Niyonzima zilipanguliwa na makipa wa timu hiyo, Aishi Manula pamoja na Emmanuel Mseja.

Wachezaji wengine ambao katika mazoezi hayo walionyesha kiwango duni katika upigaji wa penalti walikuwa ni James Kotei, Method Mwanjale pamoja Laudit Mavugo.

Akizungumzia hali hiyo, Kocha Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog alisema kuwa: “Mapungufu hayo nimeyaona lakini lakini nitahakikisha nayafanyia kazi ili wote kwa pamoja waweze kuondokana na tatizo hilo.

“Lakini ikitokea katika mechi yetu tukapigiana penalti na Yanga kuna wachezaji wengi wanaoweza kupiga na kutuwezesha kupata ushindi,” alisema Omog.

Mara ya mwisho timu hizi kukutana Simba walishinda mabao 2-1, kwenye mchezo wa ligi kuu.


BENCHI la Ufundi la Yanga, limesema kuwa leo Jumatano linaanza kuhesabu makombe ya msimu wa 2017/18 kutokana na kuwa na uhakika wa kuifunga Simba.

Leo Jumatano katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam  Yanga itapambana na Simba ukiwa ni mchezo wa Ngao ya Jamii kuashiria kufunguliwa kwa msimu wa 2017/18.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Dismas Ten, amesema kutokana na maandalizi mazuri waliyoyafanya kisiwani Pemba, wana uhakika wa kuibuka na ushindi dhidi ya wapinzani wao, Simba.

“Mechi yetu na Simba tuna uhakika wa kushinda kutokana na maandalizi tuliyoyafanya, tumejiandaa tayari kwa kuanza kuhesabu makombe msimu wa 2017/18, hakuna mtu wa kuzuia jambo hilo.

“Benchi la ufundi chini ya kocha George Lwandamina, limetuhakikishia kwamba wachezaji wote waliokwenda kambini Pemba wapo vizuri kiafya tayari kucheza mechi hiyo, inafahamika tangu zamani kwamba Obrey Chirwa, Geofrey Mwashiuya na Benno Kakolanya watakosekana kutokana na majeraha mbalimbali waliyonayo,” alisema Ten.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget