Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

“Maulid ya Mtume (s.a.w.w) inafundisha kupinga Ugaidi,Dhulma na Amani” Maulana Sheikh Jalala



Kiongozi Mkuu wa Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania Maulana Sheikh Hemed Jalala akiongea katika Maulidi hiyo, Dar es salaam.

Kiongozi Mkuu wa Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania Maulana Sheikh Hemed Jalala amewataka Watanzania kuhuisha kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) kwani Maulid inafundisha kupinga Dhulma, Ugaidi na Umuhimu wa Amani.
 
“Moja ya funzo ilikuwa ni kupambana na dhulma, na ndio maana Mtume akasema Msaidie ndugu yako akiwa amedhulumu au akiwa amedhulumiwa, kubwa ni kupinga vita dhulma, dunia leo hakuna shaka kuwa imegubikwa na dhulma katika Nyanja zote, ili kuiondoa dhulma tunaihitajia vikao hivi vya Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w).” amesema Sheikh Jalala

Sheikh Jalala amesema hayo leo katika Sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) imeyofanyika katika ukumbi wa Urban Rose Hotel, Jijini Dar es salaam.


Aidha Sheikh Jalala amesema kuwa tunapokuwa tunakumbuka kuzaliwa Mtume Muhamad (s.a.w.w)tunasoma mafundisho yake yalikuwa yanapinga aina zote za Ubaguzi.


“Dunia leo imegubikwa na kuwafanya watu kuwa wanyonge, kuwagawanya watu katika matabaka, ubaguzi bado upo hata kama ni wa kifikra bado unatawala dunia, Mtume Muhammad (s.a.w.w) alipambana na Ubaguzi.”


“Mtume Muhammad (s.a.w.w) alikuja kuwafundisha watu kuwa watu wote wako sawa, leo dunia imekuja kuwagawanya watu, watu wa ulimwengu wa tatu, ulimwengu wa pili, watu wenye haki ya kumiliki, watu wasiokuwa na haki ya kumiliki, watu wanaofaidika na rasilimali walizonazo, watu wasiofaidika na rasilimali walionazo” amesema Sheikh Jalala



Sheikh Jalala amesema kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) katika mafunzo aliyoyafunza ni funzo la amani, kwamba Mungu tunaemuabudu ni Mungu wa Amani kwa mungu siku zote inatoka Amani, leo tunaona kwa pamoja mashariki ya kati na dunia kwa ujumla imegubikwa na kitu kinachoitwa ugaidi, imegubikwa na ukatili kupita kiasi, imegubikwa ni kuchinjana ni mateso hujawahi kuyaona hata kuyasikia katika maisha yako.


“Niseme kwa masikitiko makubwa kauli ya Raisi wa Marekani Donard Trump yakuufanya Mji mtakatifu wa Palestina Masjid Aqswa mji mtakatifu wa Jerusalem, ambapo ndani yake kuna Qibla ya Waislamu kuufanya mji mkuu badala ya Teleavivi hiki ni kinyume na ubinadamu na nikinyume na tofauti katika kuenzi Amani, kupenda watu kukaa vizuri, wakae kwa salama”.Amesisitiza Sheikh Jalala
Kadhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam amabae ni Imam Mkuu wa Msikiti wa Manyema Sheikh Hamid Jongo akiongea na Waandishi.


Kwa Upande wake Kadhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambae pia ni Imam Mkuu wa Masjid Manyema Sheikh Hamid Jongo amewataka watanzania kulinda na kuienzi amani, utulivu na mshikanamo tulionao waislamu na wakristo hapa nchini.

“Natoa wito kwa watanzania hivi tulivyo amani, ushirikiano na utulivu tuupiganie kwani hii ndio jihadi yetu kuhakikisha vitu hivi vinadumu amani, utulivu na mshikamano na kuishi kwa kuridhiana baina ya watu wa dini zote” amesisitiza Sheikh Jongo.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget