Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

SAUTI JAMII KIPUNGUNI YAENDESHA KAMPENI KABAMBE YA KUPINGA UKEKETAJI KATIKA KATA HIYO


Watoto kutoka mitaa mbalimbali ya kata ya Kipunguni wakilifuata gari la matangazo la Sauti Jamii Kipunguni na kuzipokea kwa furaha huduma mbalimbali zilizokuwa zikitolewa ikiwa ni kugawa vipeperushi na kutoa elimu bure, mapema jana katika uzinduzi wa kampeni ya Akeketwi mtu mwaka 2018.
Mchungaji wa kanisa la Sinai Pentecostal Ndugu. Imani Juma Feruzi akibandika karatasi yenye ujumbe(posters) katika pikipiki mapema jana, katika uzinduzi wa kampeni ya akeketwi mtu mwaka 2018 iliyoandaliwa na Sauti Jamii Kipunguni ili kupinga vitendo vya Ukeketaji na Rushwa ya ngono.

Mwanaharakati wa Sauti Jamii Kipunguni Bi. Tausi Msangi akibandika karatasi yenye ujumbe(posters) katika moja ya duka la dawa linalopatikana katika kata ya kipunguni, mapema jana katika uzinduzi wa kampeni ya Akeketwi mtu mwaka 2018.
Wanaharakati wa Sauti Jamii Kipunguni wakiwa na watoto mbalimbali wa kata ya hiyo wakiwa wameshika mabango yenye jumbe tofauti tofauti kuashiria kuchoshwa na vitendo vya ukeketaji vilivyoshamili katika kata hiyo, mapema jana katika uzinduzi wa kampeni ya Akeketwi mtu mwaka 2018.

Mkurugenzi wa Sauti Jamii Kipunguni Bw. Selemani Bishagazi akigawa vipeperushi kwa wakazi mbalimbali wa kata ya Kipunguni eneo la Machimbo, katika uzinduzi wa kampeni ya akeketwi mtu mwaka 2018 mapema jana jijini Dar es salaam.
Wanaharakati wa kata ya kipunguni wakicheza kwa pamoja na watoto wa kata hiyo mara baada ya kuwapa elimu juu ya kupinga ukeketaji na rushwa ya ngono mapema jana jijini Dar es salaam.

Wanaharakati wa kata ya Kipunguni wakiwa katika picha ya pamoja mapema jana jijini Dar es salaam.


Na Vicent Macha

Kituo cha sauti jamii Kipunguni jana tarehe 29 mwezi desemba kimezindua kampeni mahususi ya kutoa elimu mtaa kwa mtaa, iliyofuatiwa na zoezi  kugawa vipeperushi pamoja na kubandika karatasi zenye jumbe mbalimbali katika kata hiyo.

Akiongoza kampeni hiyo Mkurugenzi wa Sauti jamii Kipunguni Bw. Selemani Bishagazi alisema kuwa lengo kuu la kampeni hiyo kuangazia sehemu kuu mbili ambazo ni kupinga ukeketaji katika kata hiyo lakini pia rushwa ya ngono katika jamii ya kitanzania.

Aidha Bw. Bishagazi alidai kuwa kampeni hiyo imelenga kupinga vitendo vya ukeketaji ambavyo vinavyotarajiwa kutekelezwa mwakani 2018 kwani ndio mwaka mahususi kwa kukeketa hususani kwa makabila yanayotokea mkoani mara ambayo yameshamili katika kata hiyo.

Aliendelea kusema kuwa watekelezaji wakuu wa mambo haya ni watu tunaoishi nao katika jamii zetu na kesi zake zinakuwa ngumu kusikilizwa kutokana kwamba watekelezaji wa hayo ni baba, mama au shangazi hivyo inaleta ugumu katika kutoa ushahidi na mtoto anaogopa kwa kuwa anajua mzazi wake au ndugu yake atafungwa kwa sababu yake.

“Wanaharakati wengi wamekuwa wakisubiri zoezi la kukeketa lianze ndipo waanze kuwakamata wahusika wakiwa tayari wameshakeketa, lakini kwetu sisi tumeona tuzuie kabla watoto hawa hawajafanyiwa ukeketaji ili kuweza kuwakomboa juu ya mila na tamaduni mbaya kama hizi” alisema bishagazi

“Kampeni hii itakuwa ni endelevu lakini pia tutajaribu kuwa karibu na wananchi ili waweze kutupa taarifa mbalimbali kuhusu wakeketaji na tutakaa nao chini tutajaribu kuwapa elimu juu ya madhara ya ukeketaji ili waachane na mambo hayo ya kizamani na mila potofu ya kukeketa na waweze kuwa watu wema katika jamii”. Alisema Mkurugenzi huyo

Lakini pia katika maeneo mengi hususani maeneo ya kazi, vyuoni, mashuleni maeneo ya biashara wananchi wanalazimishwa sana kutoa rushwa ya ngono ili waweze kupata huduma stahiki wanayohitaji, ndio maana sauti jamii kipunguni imeamua kuanzisha kampeni hii ya kupinga rushwa ya ngono katika jamii zetu.

Sauti jamii kipunguni kwa kushrikiana na mashirika rafiki kama Global Fund na TGNP na mengineyo tutawezeza kutoa elimu kwa wananchi na kuwawajibisha waajili, madaktari, walimu na watu wote walio katika sekta za Umma na binafsi ili waweze kupinga na kutoa taarifa kwa vyombo husika endapo wataombwa rushwa ya ngono watu hao.

                          ANGALIA VIDEO HII KUJUA KILICHOENDELA ZAIDI...

                  
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget