Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Donald Trump amuonya Kim Jong-Un moja kwa moja

US President Donald Trump speaks at the National Assembly on 8 November 2017 in Seoul, South KoreaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMr Trump also addressed Mr Kim directly in his speech
RAIS  wa Marekani Donald Trump ametoa onyo kali kwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong un katika hotuba ndani ya bunge la Korea Kusini.
''Usitudharau, usitujaribu," alisema, huku akishutumu hali ilivyo nchini Korea Kaskazini.
Rais  Trump alimzungumzia moja kwa moja rais Kim akisema kuwa ''silaha unazojilimbikia hazikufanyi wewe kuwa salama lakini zinakuweka katika hali hatari''.
Kiongozi huyo wa Marekani yuko katika ziara ya siku mbili nchini Korea Kusini katika ziara ya bara Asia.
Kwengineko katika hotuba yake amesema kuwa huku Korea Kaskazini ikiona uvumilivu kuwa udhaifu sasa kuna utawala mpya nchini Marekani.
Trump pia ameutaka ulimwengu hususan China na Urusi kuiwekea shinikizo kali Pyongyang kusitisha utengenezaji wake wa silaha za kinyuklia.
Dunia haiwezi kuvumilia hatari inayosababishwa na taifa linaloongozwa na utawala usioaminika ambao unaitishia na silaha za kinyuklia.
Mataifa yote yaliowajibika yanafaa kuungana kuangamiza utawala wa kikatili wa Korea Kaskazini kuhakikisha kuwa hakuna mtu anayeuunga mkono, kupata usaidizi wowote ama hata kukubalika, alisema.
CHANZO BBC NEWS
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget