Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Twitter yawaruhusu watu wengi kutumia tarakimu 280 kuandika ujumbe

Twitter logoHaki miliki ya pichaREUTERS
MTANDAO wa kijamii wa Twitter imetangaza kwamba imeanza kuwafungulia watu wanaoutumia mtandao huo   uwezo wa kuandika ujumbe kwa kutumia tarakimu 280 badala ya 140.
Kampuni hiyo ilikuwa imewawezesha baadhi ya watu kutumia tarakimu hizo lakini kwa majaribio tangu Septemba lakini sasa wamesema watu wengi wataruhusiwa kuandika ujumbe mrefu.
Watakaozuiwa pekee ni wale wanaoandika ujumbe kwa Kijapani, Kichina na Kikorea ambao wanaweza kuwasilisha maelezo zaidi kwa kutumia tarakimu chache.
Ufupi wa ujumbe
Wakati wa majaribio, ni ujumbe 5% ambao ulikuwa na urefu wa zaidi ya tarakimu 140 na ni 2% uliokuwa na zaidi ya tarakimu 190, wamesema.
Lakini walioandika ujumbe mrefu walipata wafuasi zaidi, walihusiana na watu zaidi na walitumia muda zaidi katika mtandao huo.
"Tuliona kwamba watu walipohitaji zaidi ya tarakimu 140, waliandika ujumbe kwa urahisi na mara nyingi. Muhimu zaidi, watu waliandika ujumbe wa chini ya tarakimu 140 mara nyingi zaidi na ufupi wa ujumbe wa Twitter ulisalia," meneja wa bidhaa na huduma wa Twitter Aliza Rosen ameandika
Mabadiliko hayo yalipotangazwa mara ya kwanza, wengi waliyakosoa na kusema badala yake wangelipenda kuona taarifa za chuki pamoja na mashine zinazoandika ujumbe zikidhibitiwa zaidi.
Aidha, wengi walitaka ujumbe urudi kufuata historia tena, ujumbe wa karibuni zaidi ukionekana mwanzo na pia waweze kuhariri ujumbe.
Mtandao huo kwa sasa una watu 330 milioni, idadi ambayo ni ya chini ukilinganisha na 800 milioni wa Instagram na zaidi ya 2 bilioni wa Facebook.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget