Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

MKOA WA MBEYA WA ONGOZA UFAULU MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Baraza la Mitihani la Tanzania limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) leo Januari 30, 2018 ambapo kiwango cha ufaulu wa jumla umeongezeka kwa asilimia 7 ukilinganisha na mwaka jana 2016.

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde ametangaza matokeo hayo leo jijini Dar es Salaam na kusema ufaulu kwa wanafunzi umeongezeka kwa asilimia 7 ukilinganisha na matokeo ya mwaka jana.

"Jumla ya Watahiniwa 287,713 ambao sawa na asilimia 77.09%  kwa shule za kawaida na vituo vya kujitegemea wamefaulu ambao katika ya hao wasichana wapo 143,728 sawa na asilimia 75.21% wakati wavulana wapo 143,985 sawa na asilimia 79.06%. Mwaka jana wanafunzi waliofaulu mitihani ya kidato cha nne walikuwa 277,283 ambao ni asilimia 70.09% hivyo ufaulu wa jumla umeongezeka kwa asilimia 7" alisema Msonde

Mbali na hilo Msonde aliweza kuweka wazi kuwa jumla ya wanafunzi 265 wamebainika kufanya udanganyifu mbalimbali katika mitihani hiyo ambayo ilianza kufanyika Oktoba 30, 2016 mpaka Novemba 17, 2016


 Shule 10 kitaifa ambapo shule iliyoongoza  inatoka Mkoani  Mbeya.shule hizo ni 
TOP 10 YA SHULE BORA.
1. St. Francis Girls ya Mbeya
2. Feza Boys ya Dar es salaam
3. Kemebos ya Kagera 
4. Bethel Sabs Girls ya Iringa 
5. Anwarite Girls ya Kilimanjaro 
6. Marian Girls Pwani 
7. Canossa ya Dar es salaam 
8. Feza Girls ya Dar es salaam 
9. Marian Boys ya Pwani 
10. Shamsiye Boys ya Dar es salaam 
TOP 10 YA SHULE ZA MWISHO KITAIFA
10. Mtule ya Kusini Unguja
9. Nyeburu ya Dar es salaam
8. Chokocho ya Kusini Pemba
7. Kabugaro ya Kagera
6. Mbesa ya Ruvuma
5. Furaha ya Dar es salaam
4. Langoni ya Mjini Magharibi
3. Mwenge S.M.Z ya Mjini Magharibi
2. Pwani Mchangani ya Kaskazini Unguja
1. Kusini ya Kusini Unguja

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget