Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Cairo jiji hatari zaidi kwa wanawake duniani


Mji wa Cairo una wakazi 22.8 milioni Mji wa Cairo una wakazi 22.8 milioni
JIJI  la Cairo Nchini Misri ndilo hatari zaidi kwa wanawake kuishi duniani miongoni  mwa majiji duniani, utafiti wa shirika la Thomson Reuters Foundation unaonesha nimeripoti.

Jiji la London nalo ndio mji bora zaidi kwa wanawake kuishi.

Mji wa Kishasha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unafuata Cairo, nao mji wa Lagos nchini Nigeria ni wa nane kwenye orodha hiyo.
Jumla ya majiji 19 makubwa yalichunguzwa - ambayo ni majiji yenye idadi ya watu inayofika milioni kumi na zaidi.

Miongoni mwa yaliyozingatiwa kwenye utafiti huo ni unyanyasaji wa kingono, utamaduni unaowadhalilisha wanawake pamoja na upatikanaji wa huduma bora ya afya kwa wanawake, fedha na elimu.

Wataalamu katika haki za wanawake waliombwa ushauri wao wakati wa kufanywa kwa utafiti hao, miongoni mwao akiwa mwanahabari Shahira Amin, ambaye aliambia Thomson Reuters:

"Mambo yote kuhusu wanawake katika jiji hilo ni hatari. Hata kutembea tu barabarani, na hunyanyaswa sana, kwa maneno na kwa vitendo."
CHANZO BBC NEWS
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget