Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Dk. Kigwangalla aagiza TAKUKURU kumkamata Tabibu aliyekula pesa za CHF Butiama

MGAN
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Hamisi Kigwangalla amemwagiza mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Butiama mkoani Mara, Saimon Ngiliule kumsimamisha  kazi mara moja Tabibu Danieli Mtatiro wa kituo cha Afya  Kiagata kwa tuhuma za kula pesa za wanakijiji kiasi cha sh.2 milioni zilizotokana na malipo ya mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).                
   Pia Dk. Kigwangalla amemwagiza Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU) kumkamata tabibu huyo ili kuhojiwa na kuchukuliwa hatua. “Nakuagiza Mkurugenzi msimamishe kazi Bwana Mtatiro na afikishwe TAKUKURU haraka sana. Huku ni kuujumu mpango wa serikali wa kuwaletea maendeleo kupitia afya matokeo yake mtu mmoja anachukua pesa za wananchi wanaozipatia taabu hali inayowafanya wakose matibabu” amesema Dk. Kigwangalla.              
Dk. Kigwangalla ambaye yupo katika ziara ya kuimalisha sekta ya Afya Wilaya za Butiama na  Serengeti mkoa wa Mara  pia ameweza kukagua hospitali ya wilaya Butiama pamoja na kuzuru kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Dk. Kigwangalla yupo katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili Wilayani Butiama na Serengeti. ambapo anakagua vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali ikiwa katika mpango wa uboresha wa Sekta ya Afya
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget