Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Putin: Korea Kaskazini Wako Radhi Kula Nyasi Kuliko Kuacha Nyuklia


Rais wa urusi Vladimir Putin
Rais wa urusi Vladimir Putin amesema kuwa vikwazo zaidi dhidi ya Korea Kaskazini ni bure, akiongeza ni radhi wale nyasi kuliko kuachana na mpango wao wa nyuklia.

Marekani ilisema Jumatatu kuwa itapeleka azimio mpya kwa Umoja wa Mataifa la vikwazo zaidi, kufuatia hatua ya nchi hiyo kulifanyia majaribio bomu la nyuklia siku ya Jumapili.
Bwana Putin pia alisema kuwa hatua za kijeshi inaweza kuleta janga la dunia nzima.

China, mshirika mkuu wa Korea Kaskazini pia nayo imetaka kurejelewa kwa mazungumzo.
Sanctions have been exhausted.Haki miliki ya pichaREUTERS

Putin alikuwa akizungumza kwenye mkutano wa nchi za Brics ambazo ni (Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini) huko Xiamen nchini China. Licha ya Putin kuishutumu Korea Kaskazini, alisema kuwa vikwazo havitasaidia.

Siku ya Jumatatu mjumbe wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Haley, alisema kuwa vikwazo vikali vitasababisha tatizo hilo kutatuliwa kwa njia ya kidiplomasia.
Chansela wa Ujerumani Angela Merkel aliunga mkono pendekezo hilo akisema kuwa vikwazo vya haraka vinahitajika kukabiliana na tabia ya Korea Kaskazini kukiuka maazimio ya kimataifa.

Rais wa Korea Kusini Kim Jong
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget