Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

KABURU-KAMWE MTU HAPOTEI MARA MBILI,AZAM FC LAZIMA TUWAFUNGE NUSU FAINALI YA FA


Kaburu
Na.Alex Mathias
Makamu wa Rais wa Simba Geofrey Nyange Kaburu,ametamba kuwa watapata ushindi dhidi ya Azam Fc waliopangwa nao kucheza katika hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la FA Mchezo utakaochezwa April 29 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam majira ya saa 1:00 jioni.
Kaburu amesema kuwa mchezo utakuwa mgumu kwa kila timu kwani ni muhimu kwa pande zote mbili kwani atakayeweza kuingia hatua ya Fainali ya kombe hilo na hatimaye kuchukua Ubingwa moja kwa moja atakuwa amepata tiketi ya kucheza Michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika Mwakani.
“Tunajua Azam Fc wamekuwa washindani wetu wakubwa kwani ikumbukwe walitufunga mechi mbili,Fainali ya kombe la Mapinduzi na Ligi Kuu Tanzania bara,nipende kukuambia kuwa mtu hapotei mara mbili hivyo tunaamini tutashinda na kutinga hatua ya Nusu Fainali Lengo letu ni kuchukua vikombe viwili”alisema Kaburu
Simba ambao bado wapo kileleni mwa Ligi Kuu kwa kuwa na pointi 59 kwa tofauti ya mbili na wapinzani wao Yanga watakipiga na Matajiri wa jiji la Dar es salaam Azam FC ambao msimu huu hawamo katika kugombania Ubingwa wa Ligi na wanaweka nguvu zao katika kombe hili ili waweze kutinga hatua ya Fainali ili mwakani waweze kushiriki Michuano ya CAF.
Nusu Fainali ya pili ya TFF itachezwa jijini Mwanza kwenye uwanja wa CCM Kirumba wenyeji Mbao FC watawaalika mabingwa watetezi wa kombe hilo Yanga siku ya Jumapili ya April 30 mwaka huu.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget