Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

MAJALIWA:MABALOZI WA TANZANIA TANGAZENI VIVUTIO VYA UWEKEZAJI NA UTALII


KASSIM-MAJALIWA
Waziri mkuu Kassim Moajaliwa amekutana na mabalozi wa Tanzania wanaenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali kuhakikisha wanaimarisha uhusiano na kujenga urafiki kati ya nchi  wanazowakilisha kwa lengo la kuitangaza Tanzania kiuchumi,ikiwa ni pamoja na kueleza fursa za uwekezaji na utalii  zilizopo nchini.
Mabalozi wa Tanzania walioteuliwa hivi karibuni na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,kuwakilisha  Tanzania nnje ya Nchi,wamefika ofisi ya waziri mkuu mjini Dodoma kwa lengo la kumuaga na kwenda kuanza majumukumu yao katika nchi walizopangiwa.
Waziri mkuu amewaleeza mabalozi hao kuwa Tanzania inazo fursa nyingi za uwekezaji Na jukumu lao  la kwanza la  Mabalozi hao  ni kuvitangaza vivutio vilivyopo ili kuleta wawekezaji wengi TANZANIA .
Suala la ushirikishwaji sekta binafsi pia waziri mkuu amesema Tanzania imelipa kipaumbele
Waziri Mkuu alizungumzia sula la watanzania waishio nje ya nchi , aliwataka Mabalozi kuwakutanisha na kufanya nao mikutano mara kwa mara ilikujua kama wanamatatizo yanayoyapata katika nchi wanazoishi ilikuangalia jinsi gani wanaweza kusaidiwa,
Mabalozi hawa wanaenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi za QATAR,UBELIGIJI,AFRIKA KUSINI,UJERUMANI,COMORO,ALGERIA,INDIA NA ,SUDAN.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget