Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

TPDC yang’oa vikombe lukuki Mei Mosi.


tp1
Timu za michezo za TPDC zikiwa na mafuriko ya vikombe vya ushindi zilizoupata kwenye mashindano mbalimbali ya Mei Mosi.
tp2
Shamrashamra za ushindi mnono na vikombe kwenye michezo minane kati ya kumi ambayo timu za michezo TPDC ilishiriki katika mashiondano ya Mei Mosi.
………………………………………………………………………..

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) lafanikiwa kubeba vikombe vinanena na medali nne katika michuano ya mashindano ya Maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani-Mei Mosi yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ushirika Mkoani Kilimanjaro.
Katika mashindano hayo yaliyoanza tarehe 19 hadi 29 Aprili, 2017 yaliyoandaliwa na COTWU(T) yalihusisha mashindano katika michezo ya kuvuta kamba, mbio za marathon, mbio za baiskeli, bao, kalata, draft, mpira wa pete na mpira wa miguu kama sehemu ya maandalizi ya siku ya Mei Mosi.
Akizungumza na vyombo vya habari Mwenyekiti wa Michezo wa TPDC ndugu Nelson Rwechunguraalieleza kuwa timu yake imezidi kuwa bora zaidi kwakuwa mashindano yaliyopita ilifanikiwa kuchukua jumla ya vikombe vitano na medali tatu lakini katika mashindano ya safari TPDC imefanikiwa kuchukua vikombe vinane na medali nne.
“Tumeweza kuchukua kikombe cha mshindi wa wa tatu katika mashindano ya kuvuta kamba kwa wananume, kikombe cha mshindi wa pili katika mashindano ya kuvuta kamba kwa wanawake, kikombe cha mshindi wa tatu katika mbio za baiskeli kwa wanawake na kikombe cha mshindi wa pili kwa upande wa wanaume, kikombe cha mshindi wa pili katika mashindano ya marathon kwa wanaume na kikombe cha mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume na kikombe kwa mshindi wa tatu katika mchezo wa draft’’ alieleza  mwenyekiti wa TPDC.
Kwa mujibu wa ndugu Rwechungura wafanyakazi wa TPDC walioipatia timu vikombe ni Diana Byonge na Peter Ngalu kwa upande wa baiskeli, Neema Mdegela na Darush Shija kwa upande wa mbio ndefu na Diana Byonge katikamchezo draft.
Aidha akizungumzia kushindwa kuchukua ubingwa wa mpira wa miguu, Mwenyekiti alieleza kuwa pamoja na kufungwa na timu Geita Gold Mining, kwake yeye timu yake ndiyo bingwa wa mashindano kutokana na mpira mzuri walioonyesha katika mtanange huo pamoja na kuwa pungufu kwa muda mrefu.
“Pamoja na kushindwa kuchukua ubingwa wa mpira wa miguu, bado kwangu mimi naichukulia timu yangu kama ndiye bingwa wa mashindano hayo kwakuwa tumecheza kwa kiwango bora zaidi na hata watazamaji wameshuhudia hilo na hivyo tumepata faraja na pia tunawapongeza Geita kwa ushindi walioupata ingawa changamoto zilikuwepo kwa upande wa maamuzi lakini ndio mchezo na tunatumaini zitafanyiwa kazi katika mashindano yajayo’’ alieleza mwenyekiti.
Kwa upande wake Kapteni wa timu ya mpira wa miguu TPDC ameeleza kuwa hatua waliyofikia ya kuwa washindi wa pili ni ya kumshukuru Mungu kwakuwa timu bora zilikuwa nyingi lakini ‘wao walifanikiwa kufika hatua ya fainali.
“Kiukweli najivunia kuwa na timu bora zaidi kwenye mashindano haya na hiiimedhihirishwa na ushindi tuliokuwa tukiupata hadi kufikia hatua na tumecheza vizuri saana pamoja ya kuwa pungufu kwa zaidi ya dakika 76 lakini bado tumeweza kuwadhibiti wa pinzania wetu kwa muda mrefu hadi walipoweza kutufunga gori la pili ambapo hadi mwisho wa mchezo tulitoka gori mbili kwa moja’’ alichambua kapteni wa TPDC.
Aidha alisisitiza kuwa waajiri wanapaswa kuzingatia na kusisitiza michezo kwa wafanyakazi ili kuboresha afya za wafanyakazi, kuleta umoja na kutangaza shughuli za Mashirika kwa wananchi.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget