Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

KUELEKEA KUIVAA AZAM FC NUSU FAINALI YA FA,SIMBA FULL KUJIAMINI NA ULINZI WAIMARISHWA KAMBI YA MORO

azam-vs-simba_nsvtm3ugt43k191l1ftwpdoo4
Kikosi cha Simba chini ya kocha wake, Joseph Omog kimeendelea na mazoezi mjini Morogoro kujiandaa na mechi yao ya keshokutwa ya Kombe la Shirikisho jijini Dar es Salaam.
Simba itakuwa mwenyeji wa Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mechi inayotarajiwa kuwa ngumu.
Mratibu wa Simba, Abbas Ally ‘Gazza’, amesema wanaendelea na maandalizi vizuri na uongozi unatimiza majukumu yake kuhakikisha vijana wanafanya vizuri.
“Kila kitu kinakwenda vizuri, kila kitu kipo kamili na hakika vijana wanajituma kweli. Lengo ni kufanya vizuri katika mechi hiyo,” alisema.
“Kila mmoja wetu anajua ni mechi ngumu na muhimu, hivyo kikubwa ni kuendelea kujituma kwa juhudi zaidi.”
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget