Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

YANGA YAFUNGUA AKAUNTI KWA AJILI YA WANACHAMA NA MASHABIKI KUICHAGIA PESA TIMU YAO


wpid-Boniface-Mkwasa
Uongozi wa Klabu ya Yanga umewataka wanachama na wapenzi wa timu hiyo kongwe hapa nchini kuichangia kwa hali na mali katika kipindi hiki ambacho wamekumbwa na matatizo ya kifedha tangu Mwenyekiti wake, Yusuf Manji apate matatizo.
Hayo yamesemwa na Katibu wa timu hiyo, Boniface Mkwasa leo Jumatatu baada ya uongozi wa timu hiyo kuingia makubaliano na Kampuni ya Selcom kwa ajili ya kuendesha zoezi maalum kwa ajili ya wanachama wa timu hiyo kuweza kuichangia timu yao.
“Tumeingia makubaliano na Selcom kwa miezi mitatu ya kutuendeshea zoezi la wanachama wetu kutuchangia fedha kwenye kipindi hiki ambacho tumekuwa na matatizo kidogo juu ya fedha am,bapo makubaliano hayo yataendelea zaidi baada ya kuona faida ambayo tutaipata katika wakati huo.
“Wanachama watachangia klabu kwa njia ya mitandao ya simu kupitia huduma za kutuma fedha kwa njia ya kimtandao, ambapo kwa sasa tunawaomba wanachama na mashabiki wote kuichangia timu kwa vile wanavyoweza,”alisema Mkwasa.
Mkwasa aliitaja namba ya kuchangia ni 150334 ambayo watumiaji wa mitandao yote ya simu za mkononi wanaweza kuitumia kuchangia klabu yao.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget