
Baraza la Wafanyakazi 
linaundwa kwa mujibu wa matakwa ya kisheria ya uwepo wa Baraza la 
Wafanyakazi mahali pa kazi ambalo linaendesha shughuli zake kwa 
kuzingatia Mkataba wa Baraza la wafanyakazi.
Kwa kutambua hilo, Naibu 
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Jinsia,Jinsia 
Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamis A. Kingwangala amefungua Mkutano wa 
Baraza la Wafanyakazi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii uliofanyika 
Ukumbi wa Mikutano wa Chuo Kukuu cha Dodoma kwa ili kujadili na kutoa 
maoni kuhusu utekelezaji wa majukumu ya wizara kwa mwaka 2016/17 na 
mpango na bajeti ya wizara 2017/18.
Akifungua mkutano huo, Mgeni 
rasimi Mhe. Kigwangalla alipongeza viongozi  wa TUGHE kuanzia ngazi ya 
Tawi hadi Taifa kwa kudumisha mahusiano rafiki mahala pa kazi, na kuweza
 kutoa ushauri ambao umesaidia kuaminiana na kuimarisha mahusiano baina 
ya menejimenti na wafanyakazi wa Wizara.
Mhe. Naibu Waziri ametoa rai 
kuwa, ili kufikia dira, dhima na malengo ya Wizara tunahitaji kuwa na 
mpango na bajeti inayozingatia utekelezaji wa vipaumbele vilivyowekwa. 
Kwa kutambua hilo Bajeti ya Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii imeaandaliwa
 kwa muktadha huo, na pia inaakisi sera, mipango, mikakati ya Taifa, 
Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala na mikataba ya Kikanda na Kimataifa.
Katika kufanikisha malengo 
hayo ya Mhe. Naibu Waziri amesisitiza kila mtumishi kufanya kazi kwa 
bidii na maarifa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi 
wa umma. Na pia Wizara amesisitizwa kuendelea kutoa motisha kwa 
watumishi wanaowajibika, wabunifu na wenye maadili mema ili kuwa 
kichocheo cha ubunifu, tija na ufanisi sehemu ya kazi.
Naibu Waziri ameipongeza 
Wizara kwa kufanikiwa kuandaa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi na 
kuwataka kutumia weledi na umahiri wa watumishi kukabiliana na 
changamoto zilizopo na kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara 
ambayo ni pamoja na kuelimisha jamii kuondokana na mila na desturi zenye
 madhara kama ukeketaji ambao sasa tuna asilimia 10 na ndoa za utotoni 
asilimia 37; kuamsha ari ya jamii kushiriki katika shughuli za maendeleo
 na ustawi wao; kufanya ufuatiliaji wa mashirika Yasiyo ya Kiserikali 
ili kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na taratibu. Aidha, 
ameelekeza Wizara kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa 
Kudhibiti Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao 
tumejipangia kupunguza ukatili kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2025.
Mhe. Kigwangala amebainisha 
mambo manane ambayo Wizara inatakiwa kuyazingatia. Mambo hayo ni 
kutimiza haki na wajibu kwa kila mtumishi kutoa mchango wa mawazo na 
ushauri kwenye utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/17 na Mpango na 
Bajeti ya mwaka 2017/18. Pili, kushiriki kujadili changamoto za 
kiutekelezaji na kuzibadili kuwa fursa kwa kutoa ushauri na mapendekezo 
ya namna ya kuboresha utendaji. Tatu, kutekeleza majukumu kwa mujibu wa 
sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma. Nne, kuitikia 
utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake 
na Watoto kusimamiwa ipasavyo na shirikishwa wa wadau wote.
Maeneo mengine ni kuhakikisha 
kuwa Wataalam wa wizara wanashirikiana na OR TAMISEMI ili kuhuisha ari 
ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo yao. Sita, kuimarisha 
mahusiano na OR TAMISEMI ili kuhakisha wataalam waliopo kwenye ngazi za 
Mikoa na Halmashauri wanatumika na kutekeleza majukumu ipasavyo. Saba, 
Vyuo vya maendeleo ya jamii kutoa elimu inayoandaa wataalam wenye weledi
 na mahiri katika kutekeleza kazi za maendeleo ya jamii. Mwisho, 
Watumishi kuwa na hadhari na tabia hatarishi zinazopelekea maambukizi ya
 ukimwi na kwa upande mwingine mwajiri aendelee kutoa huduma kwa 
wathirika kwa mujibu wa bajeti.
Mapema akimkaribisha Mgeni 
Rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee 
na Watoto, Bibi Sihaba Nkinga alimfahamisha Mgeni Rasimi kuwa, wajumbe 
wa Baraza la Wafanyakazi watajadili Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa Fedha 
2017/18.  Kwa mujibu wa Sheria inayounda mabaraza ya wafanyakazi mahali 
pa kazi kwani ni lazima Bajeti ya Wizara ipitishwe na Baraza la 
Wafanyakazi.  Agenda ya pili, ilikuwa kupitia na kufanyia marekebisho 
muundo wa Baraza ili kujumuisha Idara ya Ustawi wa Jamii, 
iliyounganishwa kutoka Idara Kuu ya Afya, baada ya mabadiliko ya muundo 
wa Wizara.  Aidha, baada ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi kuhamia 
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Wizara imeona kuna umuhimu wa 
kuwa na wawakilishi wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii 
kwa uwakilishi wa menejimenti na uwakilishi wa watumishi.
Katibu Mkuu Sihaba, alifafanua
 tunu za Wizara kwamba, ari waliyonayo watumishi katika kutimiza 
majukumu yao kwa weledi, uadilifu, juhudi na maarifa katika kuchangia 
maendeleo na ustawi endelevu wa Taifa. “Katika hili tumeendelea 
kuhamasisha jamii na kutoa elimu kuhusu maendeleo na ustawi wa jamii, 
usawa wa kijinsia, uratibu wa mashirika yasiyo ya kiserikali na 
maendeleo ya mtoto kwa jamii, maafisa wa serikali na wadau wengine wa 
maendeleo”. alisema.
Kitengo cha Mawsiliano Serikalini
Wizara ya Afya, Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Idara Kuu ya Mendeleo ya Jamii
Post a Comment