Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Mbunge amkosoa rais Magufuli

Na Suleiman Msuya, Lindi

MBUNGE wa Jimbo la Mchinga mkoani Lindi, Hamidu Bobali amesema kitendo cha Serikali kulazimisha mapato ya halmashauri kukusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kitaua halmashauri nchini kwa kukosa mapato.

Bobali aliyasema hayo wakati akichangia bungeni Bajeti ya Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) ambayo imewasilishwa na mawaziri husika.

Alisema uamuzi wa Serikali kuu kukusanya mapato ambayo yanapaswa kukusanywa na halmashauri utaathiri ufanisi katika ofisi hizo na kukwamisha miradi mbalimbali.

Alisema Serikali kuu kupitia TRA ilitangaza kukusanya kodi ya majengo ambapo matokeo yake ukusanyaji katika Manispaa ya Kinondoni umeshuka kutoka lengo la sh, bilioni 29 hadi sh. bilioni 4.

Mbunge huyo alimtaka waziri husika kutafakari kabla ya kuchukua uamuzi ambao anapatiwa na mawaziri wenzake akitolea mfano ushauri wa kukubali kodi ya majengo ikusanywe na TRA.

Bobal alisema amechunguza katika nchi mbalimbali ambazo zinaendeshwa kwa mifumo inayofanana na Tanzania lakini hazikusanyi fedha kwa mfumo huo.

“Mapato hayakusanywi ipasavyo kutokana na TRA kuingilia mamlaka ambazo si zake na sijui kwanini waziri wa Tamisemi alivyoshauriwa hakushirikisha ushauri kutoka nje leo hii mapato yanakosekana na dalili za kufa kwa halmashauri zipo,” alisema.

Aidha, mbunge huyo amehoji ni vigezo gani vinatumika kwa wakuu wa wilaya kuondoa Serikali za Vijiji madarakani akitolea mfano mkuu wa wilaya ya Dodoma hivi karibuni aliagiza mwenyekiti aondoke na kuhoji je hayo ni maagizo ya Rais.

Mbunge huyo aliomba Serikali kuwapatia watumishi wa idara ya afya ambapo alibainisha kuwa vipo vituo vinne vipya ila havina wafanyakazi.
Bobali alisema pamoja na agizo la Rais John Magufuli ambalo alilitoa katika ziara yake ambayo aliifanya katika mkoa huo bado utekelezaji umeshindika.


Aidha, alisema mkoa wa Lindi unakabiliwa na uhaba wa walimu jambo ambalo linachangia wanafunzi kufeli katika mitihani kuanzia msingi na sekondari.

Kwa upande mwingine mbunge huyo ameitaka Serikali kuachana na mpango wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) kama hauwezi kufikia jamii kubwa zaidi.

Alisema Tasaf inapatikana katika tarafa chache akitolea mfano katika jimbo lake ambapo katika tarafa nne ni tarafa mbili zinapata.
Aidha, ameitaka Tamisemi kukemea baadhi ya wakurugenzi ambao wameonesha kushindwa kuendana na kasi ya utumishi wa umma kutokana na kukosa mafunzo.


Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget