Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDI AFUNGA KIKAO CHA BARAZA LA WAWAKILISHI

bas1
Waziri wa Kilimo,Maliasili Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid kushoto akibadilishana mawazo na Waziri wa Fedha  na Mipango Dk,Khalid salum Mohammed  katika baraza la Wawakilishi Zanzibar.PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR
bas2
Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma akibadilishana mawazo na Muakilishi wa Jimbo la Kikwajuni Nassor Salim Ali katika baraza la Wawakilishi Zanzibar.
bas3
-Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Ufungaji wa Baraza la Wawakilishi ilioambatana na uchambuzi wa masuala mbalimbali yaliojadiliwa katika baraza hilo Mbweni Zanzibar.
bas4
-Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Ufungaji wa Baraza la Wawakilishi ilioambatana na uchambuzi wa masuala mbalimbali yaliojadiliwa katika baraza hilo Mbweni Zanzibar.

……………………………………………………………
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka Wananchi ambao wanadai kuchukuliwa maeneo yao kufuatia zoezi la kuzuia Mchanga wawasilishe Vielelezo vyao katika Taasisi husika ili kufanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika hotuba yake ya kuahirisha kikao cha Tisa cha Baraza la Wawakilishi mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Amesema hatua iliyochukuliwa ilikuwa na lengo la kuweka utaratibu mzuri wa matumizi bora ya Mchanga ambao kadri unavyotumika unaendelea kumalizika.Balozi amesema Serikali imeandaa utaratibu ambao kama utafuatwa vyema utaweza kuinusuru Zanzibar na uhaba wa mchanga kwa vizazi vya sasa na baadae.
Kuhusu malalamiko yanayotolewa na Wananchi juu ya utendaji wa Hospitali Kuu ya Mnazi mmoja Balozi amesema kuanzia sasa Serikali haitomvumilia mfanyakazi yeyote atakayefanya uzembe na hatua kali za kinidhamu ama kufukuzwa kazi zitachukuliwa dhidi yake.
Amesema yapo malalamiko kuwa baadhi ya madaktari hushindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo na kuwatolea lugha chafu wagonjwa jambo ambalo si haki na halivumiliki tena.Amesema dhamira ya Serikali ya Mapinduzi chini ya Dkt Ali Mohamed Shein ni kutoa huduma bora za afya nchini na kuahidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyobainishwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa uzito wake.
Kuhusu Michezo Balozi Seif amesema Serikali inaendelea na juhudi zake za kuimarisha michezo nchini na kuwapongeza waliosaidia harakati za Zanzibar kupata uanachama wa kudumu wa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF).
Amesema kufuatia Zanzibar kupata uanachama huo wa CAF kunaashiria uwezekano mkubwa pia wa kupata Uanachama wa FIFA hali ambayo itapelekea Vijana kushiriki katika mashindano ya kimatifa.Ameongeza kuwa tayari hatua za awali za kuomba uanachama wa FIFA  zimeshaanza kuchukuliwa na Serikali na kwamba kazi iliyonayo ni kuwaandaa Vijana kushiriki mashindano hayo.Katika Mkutano huo wa tisa Baraza lilijadili na kupitisha Bajeti ya serikali ambapo pia jumla ya maswali 169 ya msingi na Maswali 418 yanyongeza yaliulizwa na kupatiwa majibu. Aidha mkutano huo ulijadili jumla ya Miswada mitano na kuipitisha kuwa sheriaKwa upande wake Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid aliwataka wajumbe wa Baraza hilo kurudi Majimboni mwao kutekeleza kwa vitendo waliyoyapanga.Mkutano huo wa Tisa wa Baraza la Wawakilishi umeahirishwa leo June 23 hadi Jumatano ya Septemba 27, 2017.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget