Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

UWASA WAPONGEZA JITIHADA ZA JPM KATIKA SEKTA YA MISITU

pic+uwasa
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Umoja wa Wavunaji Sao Hill (UWASA) pamoja na Wadau wa mazao ya miti wamepongeza jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli za ugawaji wa malighafi za misitu  kwa wenye viwanda vya mbao.

Akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa UWASA, Christian Ahia pamoja na wadau wa mazao ya miti  wamesema kuwa hatua hiyo itawasaidia katika  kuboresha na kupanua soko la mbao hapa nchini.
“Tunaipongeza  serikali kwa hatua nzuri iliyofikia ambapo imetoa vibali 421  kwa wawekezaji wa viwanda vya kuchakata mbao huko Mafindi mkoani Iringa, ukilinganisha na    vibali 1,000  vilivyokuwa vimetolewa awali kwa watu ambao hawakuwa na wawekezaji halali wa mbao” alisema Ahia.
Naye, Katibu Mkuu wa UWASA, Dkt.  Bazil Tweve  alisema kuwa, serikali ina misitu zaidi ya 15 nchi nzima,  ambapo msitu wa Sao hill   unazalisha asilimia 95 ya mbao zote zinazotumika  nchini,  hali ambayo ilisababisha uhaba wa malighafi katika viwanda vya kuchakata mbao kwa vile baadhi ya wavunaji hawakuwa na sifa na vigezo vya kufanya shughuli hiyo.
“Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kutoa vibali 421 kwa viwanda vya kuchakata mbao, tunaishukuru serikali na kuipongeza kwa hatua hii muhimu ya kuona tija ya viwanda na sisi tunaahidi kufanya shughuli zetu kwa kufuata taratibu na sheria zilizowekwa alisema Dkt Tweve.
Hapo awali kabla ya upembuzi yakinifu wa kubaini wawekezaji halali wa kuchakata mbao, kulikuwa na uhaba wa malighafi ambao ulisababishwa na utaratibu usiofaa wa ugawaji wa malighafi hizo.
Licha ya pongezi hizo kwa serikali UWASA imesema inakabiliwa na changamoto za masoko ya mbao zinazochakatwa nchini, na hivyo wameiomba serikali kuwasaidia kutafuta soko ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuuza bidha zao.
Aidha, changamoto nyingine inayowakabili UWASA ni kiwango kikubwa cha kodi zinazotozwa na Mamlaka ya Mapato (TRA) pamoja na Halmashauri ambapo wameziomba Mamlaka husika kuwapunguzia  kiwango cha kulipa tozo hizo.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget