Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

WAZAZI WENYE WATOTO WALEMAVU WAASWA KUACHA KUWATELEKEZA/KUWANYANYAPAA


unnamed
MWENYEKITI wa chama cha waandishi wa habari wanawake mkoani Pwani,(PWMO),Mwamvua Mwinyi,akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na halmashauri ya Chalinze na chama hicho,uliolenga kutoa sauti ya pamoja kukemea vitendo vya unyanyasaji kwa watoto. 
1
MTOTO mwenye ulemavu Ibrahim Ramadhani ,alietelekezwa na mama yake mzazi akiwa na miezi tisa ambapo kwasasa akisoma shule ya msingi Miono,akitoa ushuhuda baada ya kusaidiwa kibaiskeli cha kutembelea,katika mkutano ulioandaliwa na halmashauri hiyo,na chama cha waandishi wa habari wanawake mkoani Pwani (PWMO),uliolenga kuzungumzia masuala ya ulinzi na haki za watoto .

2
Mwenyekiti wa halamashauri ya Chalinze ,Saidi Zikatimu mwenye kibagharashia akiongea na mtoto mwenye ulemavu Ibrahim Ramadhani ,alietelekezwa na mama yake mzazi na sasa akisoma shule ya msingi Miono,katika mkutano ulioandaliwa na halmashauri hiyo,na chama cha waandishi wa habari wanawake mkoani Pwani (PWMO),uliolenga kuzungumzia masuala ya ulinzi na haki za watoto .
…………………
Na Mwamvua Mwinyi,Chalinze
WAZAZI,walezi na jamii kijumla ,imetakiwa kujenga upendo kwa watoto wenye ulemavu pasipo kuwatelekeza ama kuwanyanyapaa, hali inayosababisha kuwakosesha haki zao za msingi ikiwemo elimu.
Aidha halmashauri ya Chalinze imeombwa ,kutenga fedha kwa ajili ya kuwezesha watoto wenye ulemavu pamoja kuweka miundombinu rafiki katika katika shule za msingi na sekondari zinazojengwa.
Mratibu kituo cha walimu ,kata ya Miono Christopher Rutuku ,alisema hayo katika mkutano ulioandaliwa na halmashauri hiyo,na chama cha waandishi wa habari wanawake mkoani Pwani (PWMO),uliolenga kuzungumzia masuala ya ulinzi na haki za watoto .

Alisema wapo baadhi ya wazazi wanaowakimbia watoto wao wenye ulemavu,kutokana na kuona aibu ndani ya jamii.

Alieleza kwamba ,yupo mtoto mwenye ulemavu wa miguu na mikono ambae ,anasoma na kuishi kwenye mazingira hatarishi ,Ibrahim Ramadhani ,amekimbiwa na mama yake mzazi.

Rutuku alisema ,mtoto huyo alikatishwa kunyonya na mama yake,,Moshi Musini Hamisi,wakati akiwa na miezi tisa hivyo kuanza kulelewa na bibi yake Asha Mbegu.

“Alipoachishwa ziwa alibakia na baba yake mzazi lakini muda mfupi kutokana na kuathirika kisaikolojia kisa kuzaa mtoto mwenye ulemavu na kugombana na mkewe nae alipata uchizi na kushindwa kuendelea kulea mtoto”

“Bibi yake alilazimika kuuza shamba lake lililopo Msata akahamia Miono kwa kuwa hana mlezi ,kwasa nafanya jitihada ya kumtafutia shule kwakuwa shule hii ya msingi anayosoma hapa Miono haina miondombinu mizuri.”alisema Rutuku.

Rutuku ,kwasasa ameamua kuchukua hatua ya kutafuta shule inayojihusisha kusaidia watoto wenye ulemavu,(kituo cha Amani- Morogoro )ambapo itamsaidia kwenda kusoma katika mazingira rafiki na bora .

Hata hivyo alisema inatakiwa kiasi cha sh.700,000 ili aweze kuchukuliwa na kituo hicho  ambapo yeye hana uwezo wa kumpeleka hivyo anaomba msaada kwa wadau mbalimbali.

“Mnamuona huyu mtoto alivyo hawezi kutembea anasota na mikono ikiwa ina tatizo,mtoto wa wenzio ndio wako tusaidie namna ya kupata fedha hizo ili aweze kupata haki yake ya msingi ya elimu”alisisitiza.

Nae mwakilishi kutoka TAMWA,Penzi Nyamungumi,alisema watoto wote wana haki ya kupata haki zao bila kuwagawa kijinsia ama kwa ulemavu wao.
Alikishukuru chama cha waandishi wa habari wanawake mkoani Pwani,kwa kuona umuhimu wa kutoa sauti moja na halmashauri ya Chalinze,kuhakikisha jamii na vyombo na taasisi mbalimbali zinakumbushwa wajibu wao wa kusimamia masuala hayo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze,Saidi Zikatimu,akizungumzia tukio la mtoto huyo,wataangalia uwezekano wa kusaidia kiasi hicho cha fedha .

Aliwataka wenye mamlaka katika kutoa haki kwa watoto kuimarisha utoaji wa haki za watoto kwa kuhakikisha wanaohusika na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia wanachukuliwa hatua.
Zikatimu alibainisha halmashauri hiyo inawalipia bima ya afya wazee 8 kwa kila kijiji,watoto wenye ulemavu 8 na wanaoishi kwenye mazingira magumu wanne.

Afisa maendeleo ya jamii halmashauri ya Chalinze Frank Makala,alisema, wanafunzi 19 wa shule za msingi na sekondari kwenye halmashauri hiyo wamekatishwa masomo baada ya kupata mimba katika kipindi cha mwaka 2016/2017.

“Watu waliohusika na kuwapa mimba wanafunzi hao kesi zao ziko kwenye hatua mbalimbali za kisheria ili hatua ziweze kuchukuliwa kwani vitendo hivyo ni kinyume cha sheria,” alisema Makala.
Alisema kuwa kati ya wanafunzi waliopewa mimba katika kipindi hicho wa sekondari ni 15 na wa shule za msingi ni wanne ambao wameshindwa kuendelea na masomo kutokana na kupata ujauzito.
Mwenyekiti wa Chama Cha waandishi wa habari wanawake mkoani Pwani,Mwamvua Mwinyi,alivitaka vyombo vya sheria,dawati la jinsia,watendaji wa vijiji na vitongoji kila mmoja kutimiza wajibu wake.

Alisema mimba za utotoni ,kulawiti na kubaka ni wimbi linaloendelea kukua hivyo pasipo jitihada hali itazidi wakati wahusika wakiendelea kutamba mitaani.
Mwamvua alitoa rai kwa waaandishi wa habari mkoa na taifa kijumla kutumia kalamu zao kutetea haki za watoto na wanawake ili kuwakomboa.

Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget