Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

SIMBA SC UWANJANI LEO MICHUANO YA SPORTPESA!

Mwagala
Washindi wa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC), Simba leo wanatupa kete yao ya kwanza kwenye michuano ya SportPesa Super Cup watakapomenyana na Nakuru All Stars Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam

Mchezo huo utaanza Saa 8:00 mchana na utafuatiwa na mchezo wa pili wa kundi hilo, baina ya Jang’ombe Boys ya Zanzibar na Gor Mahia ya Kenya hapo hapo Uhuru.
Michuano hiyo ilianza jana Uwanja wa Uhuru, mabingwa wa Tanzania wakiwang’oa mabingwa wa Kenya, Tusker FC kwa penalti 4-2 baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 90.
Awali ya hapo, vigogo wa Kenya, AFC Leopards nao waliitupa nje Singida United kwa penalty 5-4 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 90 pia.
Bingwa wa michuano hii atajinyakulia kitita cha dola za Kimarekani 30,000 zaidi ya Sh. Milioni 65 za Tanzania pamoja na nafasi ya kucheza mchezo wa kirafiki na klabu ya Everton ya England
RATIBA NA MATOKEO SPORTPESA SUPER CUP
Juni 5, 2017
Singida United 1-1 AFC Leopards (Penalti 4-5)
Yanga SC 0-0 Tusker FC (Penalti 4-2)
Juni 6, 2017
Jang`ombe Boys vs Gor Mahia
Simba Vs Nakuru All Star
NUSU FAINALI
Juni 8, 2017
AFC Leopards Vs Yanga SC
Simba SC/Nakuru All Star Vs Jangombe Boys/Gor Mahia
FAINALI
Juni 11, 2017
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget