Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Baada ya kuambiwa ngoma zake zimebuma, Ditto afunguka

Lameck Ditto.

BAADA ya ngoma zake mbili alizotoa hivi karibuni kudaiwa kubuma, staa wa Wimbo wa Moyo Sukuma Damu, Lameck Ditto ‘Ditto’ amefunguka kuwa habari hizo siyo za kweli, kwani kwa upande wake anaona ziko vizuri.

Akichonga na Risasi Vibes, Ditto alisema ngoma zake hizo ambazo ni Bembea na Nabadilika hazijabuma kwani siku zote amekuwa akifanya muziki ambao umekuwa na mashabiki wengi kwa hiyo hauwezi kukwama kwenye vyombo vya habari ‘media’ hata siku moja.

“Nimeona kwenye mitandao ya kijamii watu wakidai nyimbo zangu nilizoachia hivi karibuni zimebuma, hilo si kweli maana kama ni video nimepeleka kwenye media mbalimbali na zinapigwa kwa hiyo watu waache kuzungumza vitu ambavyo havina ukweli ndani yake,” alisema Ditto.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget