Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Idadi ya watoto wanaotumiwa kama walipuaji wa kujitolea mhanga yaongezeka Nigeria

Mourners react on July 24, 2017, in the Dalori IDP (Internally Displaced People) camp outside Maiduguri, after a suicide bomb attack that killed fourHaki miliki ya pichaAFP
Image captionThe Boko Haram insurgency has devastated many lives across north-eastern Nigeria
KUMEKUWA na ongezeko kubwa la  idadi ya watoto wanaotuhumiwa kama washambuliaji wa kujitolea mhanga na wanamgambo wa Boko Haram, kaskazini mashariki mwa Nigeria, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto Unicef, linasema kuwa tayari visa 83 vimeripotiwa mwaka huu, mara nne zaidi ya vile vya mwaka wote wa 2016.
55 kati yao walikuwa ni wasichana walio na umri chini ya miaka 15 na kwenye kisa kimoja, bomu lilifungwa kwa mtot ambaye alikuwa amebewa na msichana mdogo.
Unicef inasema mbinu hii imezua hofu kwa watoto wanaoachiliwa na Boko Haram kulingana na Umoja wa Mataifa, watoto 127 wametumiwa kama walipuaji kaskazini mashariki mwa Nigeria tangu mwaka 2014.
Wanamgambo wa Boko Haram mara kwa mara wamewatumia watoto, na wamewateka mamia ya wasichana wa shule na kuwalazimisha watoto wavulana kujiunga na jeshi lao.
CHANZO BBC NEWS
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget