Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Man Fongo anusurika kifo, adondoka juu ya paa

Amani Fongo ‘Man Fongo’.

MSANII wa muziki wa Singeli nchini, Amani Fongo ‘Man Fongo’ mwishoni mwa wiki iliyopita alinusurika kifo baada ya kutereza juu ya paa la nyumba wakati akiweka balbu ya umeme.

Akisimulia mkasa huo kwa Risasi Vibes, Man Fongo alisema tukio hilo lilitokea Sinza jijini Dar alikohamia ambako alikuwa akisimamia mafundi waliokuwa wakiifanyia ukarabati nyumba hiyo, ambapo alipoanguka, mkono wake mmoja uliingia katika chuma kimoja cha geti na kum-pasua kiasi cha kutokezea upande wa pili.

“Nashu-kuru kwa sasa naendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu, kiukweli sijui ilikuwaje mpaka nikatereza kwani nilishtukia nimedondoka na kuumia, maumivu niliyoyapata siwezi hata kuyaelezea kwa kweli,” alisema Man Fongo.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget