Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Yanga yatamba kuanza kuhesabu makombe leo


BENCHI la Ufundi la Yanga, limesema kuwa leo Jumatano linaanza kuhesabu makombe ya msimu wa 2017/18 kutokana na kuwa na uhakika wa kuifunga Simba.

Leo Jumatano katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam  Yanga itapambana na Simba ukiwa ni mchezo wa Ngao ya Jamii kuashiria kufunguliwa kwa msimu wa 2017/18.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Dismas Ten, amesema kutokana na maandalizi mazuri waliyoyafanya kisiwani Pemba, wana uhakika wa kuibuka na ushindi dhidi ya wapinzani wao, Simba.

“Mechi yetu na Simba tuna uhakika wa kushinda kutokana na maandalizi tuliyoyafanya, tumejiandaa tayari kwa kuanza kuhesabu makombe msimu wa 2017/18, hakuna mtu wa kuzuia jambo hilo.

“Benchi la ufundi chini ya kocha George Lwandamina, limetuhakikishia kwamba wachezaji wote waliokwenda kambini Pemba wapo vizuri kiafya tayari kucheza mechi hiyo, inafahamika tangu zamani kwamba Obrey Chirwa, Geofrey Mwashiuya na Benno Kakolanya watakosekana kutokana na majeraha mbalimbali waliyonayo,” alisema Ten.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget