Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

TAASISI YA BILL & MERINDA GATES YATOA USD MIL. 15 KUSAIDIA SEKTA YA AFYA.


bil4
Mwenyekiti mwenza wa Bill & Melinda gates foundation,bilionea Bill Gates akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi  wa mpango wa mfumo  wa matumizi  ya kielektroniki katika sekta ya afya  uliofanyika jijini Dar es salaam.
………………………………
NA WAMJW –DAR ES SALAAM.
TAASISI ya Bill & Melinda Gates imetoa dola za kimarekani shilingi milioni 15 ili kusaidia mpango wa matumizi ya mfumo wa kielektroniki kuimarisha upatikanaji wa huduma bora katika sekta ya afya nchini.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti mwenza wa Taasisi hiyo ambaye ni tajiri wa Dunia  Bill Gate katika uzinduzi wa mfumo huo uliofanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya afya jijini Dar es salaam wakati alipotembelea nchini Tanzania.
“Mfumo huu utasaidia na kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ,maamuzi kwa watendaji wa afya nchini Tanzania katika kutoa na kuboresha huduma kwa wananchi wao” alisema Bill Gate.
Aidha Bill Gate amesema kuwa mfumo huo utasaidia kuimarisha na kuboresha matumizi sahihi ya takwimu na kuleta matokeo sahihi katika kufuatilia sawa pamoja na taarifa za utoaji wa chanjo.
Kwa upande wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano imekua ikitilia mkazo na matokeo chanja katika kuleta ufanisi katika sekta ya afya.
“Tukiwa na mifumo mizuri ya kielektroniki tutaweza kujua dawa gani zimepelekwa katika kituo flani na kiasi gani cha dozi na aina ya dozi wamepewa wagonjwa gani” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa mfumo huo utaboresha upatikanaji na uhifadhi  wa taarifa za wagonjwa kirahisi tofauti bna zamani kwani mafaili mengi kwa sasa yanahifadhiwa kwa uhakika na usalama zaidi.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget