Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

MPINA AAGIZA UJENZI WA CHANZO CHA MAJI CHA AJABU KUKAMILIKA MAPEMA


DSC_0120
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Mhe.Luhaga Mpina ambaye pia ni Mbunge wa Kisesa akiongea na wadau hawapo katika picha kuhusu utekelezaji wa mradi wa chanzo cha maji cha Igombe, Mwandoya Mkoani Simiyu.
DSC_0106
Chanzo cha maji cha ajabu kikiwa chini ya Mchanga, ambapo juu hakuna maji yoyote yanayoonekana badala yake ni mchanga unaonekana kama mto uliyokauka maji,   chanzo hiki kipokatika kijiji cha Igombe wilayani Meatu.
DSC_0125
Jengo linaloonekana katika Picha ni sehemu ya kupokelea maji yanayotoka chini ya mchanga na kupanda bila pump katika mabomba ndani ya jengo hilo na kuja kusambazwa kwa wakazi kwa vijiji jirani kwa matumizi ya nyumbani
DSC_0097
Jengo linaloonekana katika Picha ni sehemu ya kupokelea maji yanayotoka chini ya mchanga na kupanda bila pump katika mabomba ndani ya jengo hilo na kuja kusambazwa kwa wakazi kwa vijiji jirani kwa matumizi ya nyumbani
………………….
NA EVELYN MKOKOI – IGOBE
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina ameagiza chanzo cha maji cha kipekee ambacho kinatoa maji chini ya  Mchanga, kilichopo katika kijiji cha Igobe Wilayani Meatu kukamilika ifikapo mwisho wa Mwezi huu ili kusaidia utoaji na usambazaji wa huduma ya maji safi na salama katika vijiji jirani na chanzo hicho na kata ya Mwandoya kwa ujumla.
Akiendelea na ziara ya kikazi Jimboni Kisesa, Mpina ameelezwa kuwa ucheleweshwaji wa kukamilika kwa matumizi ya chanzo hicho cha maji yametokana na kucheleweshwa kwa malipo kwa mkandarasi Mbesso Constraction Company ltd. ambapo kati ya fedha za mradi shilingi milioni 502, zinazotelewa na serikali kupitia Wizara ya maji na umwagiliaji ni kiasi cha fedha cha shilingi milioni 114 tu ndizo zilitoka na kutumika mpaka sasa.
Mpina, ameagiza kufanyiwa kazi kwa kasoro zilizojitokeza katika mradi huo wenye uwezo wa kuhudumia takribani watu elfu nane katika kijiji cha Mwandoya na Igobe,  ili kumuwezesha mkandarasi kukamilisha kazi hiyo wa wakati.
“ Lazima Pawepo na usimamizi madhubuti katika mradi huu ili wakazi wa maeneo jirani na mradi na mbali na hapa waweze kunufaika na kama kutajitokeza kwa uzembe wowote wahusika watawajibika kwa mamlaka.” Alisisitiza Mpina.
Katika ziara yake Naibu Waziri Mpina pia alitembelea shule ya Sekondari ya Mwandoya ambapo aliongea na walimu wa shule hiyo na kuwaeleza bila kuficha kuwa wamekuwa wakilaumiwa sana kwa kuwa na mauhusiano ya kimapenzi na wanafunzi wa shule hiyo na kuwaasa kuacha tabia hiyo inayopelekea kuwaharibia maisha vijana hao na kutoa wito kwa watu wazima katika kijiji cha Mwandoya kuachana kabisa na tabia hiyo kwani ni kinyume na sheria na maadili ya Tanzania na kuwa Serikali ya awamu ya tano ipo kazini.
 Pamoja na hilo Mpina alisikiliza changamoto zinazoikabili shule hiyo na kuhaidi kutatua baadhi ya changamoto mpya, pia Mpina alikagua baadhi ya Mabweni mapya ya kisasa yaliyojengwa katika shule hiyo.
Sambamba na hilo Naibu Waziri Mpina ambaye pia ni Mbunge wa Kisesa, alikagua ujenzi wa wodi Mpya ya wazazi inayojengwa katika zahanati ya Mwandoya ambayo imefikia katika hatua ya kupauliwa.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget