Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BIMA NCHINI YAWABANA WATUMIAJI WA STIKA ZA BIMA BANDIA

unnamed
ASKARI wa usalama barabarani wilayani Kibaha mkoani Pwani wakisikiliza elimu juu ya matumizi ya mfumo wa kubaini stika bandia kwa magari mbalimbali,mfumo ulianzishwa na mamlaka ya usimamizi wa Bima nchini TIRA.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
A
kamishna wa mamlaka ya usimamizi wa bima nchini,dr.Baghayo Saqware ,wa kwanza kulia akieleza jambo kwa askari wa usalama barabarani eneo la Mailmoja Kibaha.(picha na Mwamvua Mwinyi)
A 2
Jopo la wajumbe kutoka mamlaka ya usimamizi wa bima nchini wakihakiki stika za bima katika moja ya lori eneo la mizani Mailmoja Kibaha.(picha na Mwamvua Mwinyi)

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA),imeanza kampeni endelevu ya kuhakiki magari yenye stika za bima bandia ili kuondoa wimbi la stika hizo ambalo hulisababishia serikali kukosa mapato.

Aidha zoezi hilo litawezesha kubaini mtandao wa makampuni yanayotengeneza stika hizo .

Akizindua zoezi hilo mjini Kibaha,kamishna wa mamlaka ya usimamizi wa bima nchini,dr.Baghayo Saqware ,alisema kampeni hiyo itaendeshwa kwa kusimamiwa na jeshi la polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani kwa kushirikiana na TIRA.

Alieleza kwamba ,uhakiki huo utafanyika kwa kutumia mfumo wa teknolojia ya TEHAMA-unaoitwa TIRA –MIS .
Saqware alisema,askari wa usalama barabarani wanapaswa kutumia mtandao na ujumbe wa kawaida kwenda namba 15200 ambapo watapokea maelezo ya halisi ya stika anayoikagua.

Hata hivyo alibainisha kuwa,wameamua kubuni mfumo huo ili kukomesha wizi unaofanywa na baadhi ya makampuni yanayotengeneza stika na wamiliki wa magari.

Kamishna huyo alisema,tatizo hilo linaweza kukua zaidi endapo mamlaka hiyo itaendelea kukaa kimya ikiwa ni watengeneza wakuu wa stika hizo za bima.

“Tatizo ni kubwa hasa mikoa inayopitiwa na barabara kuu ya Dar es salaam ,Pwani na Arusha”

“Kutokana na hilo tumeona vyema tukaanza kujenga ufa kabla ya ukuta ,Hali isije kuwa mbaya zaidi’alisisitiza Saqware.

Saqware alielezea,wamezindua zoezi na kampeni hiyo rasmi kwa kuanzia wilaya ya Kibaha kwa kutoa elimu kwa askari wa usalama barabarani juu ya mfumo huo.

Alisema kila ofisi yao ya kanda itatekeleza zoezi hilo kwa kutoa elimu kwa wananchi,askari wa usalama barabarani na madereva.

Nae kamanda wa usalama barabarani mkoani Pwani,Abdi Issango ,alisema zoezi hilo limeanzishwa katika muda muafaka kwani utitiri wa stika feki ni kero kubwa.

Alisema wimbi la stika bandia linakwamisha mapato ya serikali na kuumiza wananchi wasio na hatia.

Kamanda Issango ,itasaidia kukamata magari yenye stika feki ili kubaini mtandao wa makampuni mbalimbali yanayotoa bima zisizo halali.

“Watu waliokuwa wakiuziwa bima bandia, kwa sasa watauziwa bima halali na watapata haki zao bila usumbufu “
“Kuna kesi nyingi za bima feki ama wamiliki wengine hutumia stika moja ya bima kwenye magari yake zaidi ya kumi,kinyume na taratibu za TIRA”alifafanua Issango.

Kamanda Issango ,alisema bima ni kinga ya ajali ,wahanga wanatakiwa kufidiwa hivyo kama gari limepata ajali halijakata bima  linamnyima mwananchi haki yake ya matibabu,majeruhi na kifo.

Alisema kwa mkoa wa Pwani hali hairidhishi ,kwani magari mengi yamekuwa yakifoji ,na kuwa na stika walizozipata kwa njia za mkato.

Kamanda Issango ,alitoa wito kwa wananchi hasa wamiliki wa mabasi,malori na magari binafsi kuacha kupitia njia zisizo halali kununua ama kutengeneza stika bandia .
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget