Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

Meya Mwita awaonya wakina Baba, asema wakina Mama waungwe mkono kwenye shuguli za maendeleo


Displaying 20170513_134048.jpg
Displaying 20170513_135157.jpg
Wakina Mama waliohudhuria semina hiyo wakimshangilia Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita alipokuwa akizungumza nao kwenye ufunguzi wa seminahiyo.
Displaying 20170513_134213.jpg
Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akizungumza na wakina Mama waliohudhuria semina hiyo.
Displaying 20170513_135525.jpg
Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita mwenye kofia katikati akizungumza jambo na Mwanaharakati wa kipindi cha Wanawake Live Joyce Kiri wa kwanza kulia , wakati wa ufunguzi wa semina ya vikundi vya wakina mama vya wanawake Live iliyofanyika Pugu jijini hapa leo.kushoto ni Diwani wa kata ya Pugu Henry Kilewo
 
CHRISTINA MWAGALA,OFISI YA MEYA WAJIJI

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema anatambua mchango mkubwa unaotokana na wakina Mama na hivyo kuwataka wa kina Baba kuwaunga mkono kwa asilimia 100 katika shuguli za maendeleo.

Meya Mwita alitoa kauli hiyo jiji hapa jana wakati wa uzinduzi wa Vikundi vya wa kina mama vya wanawake Live yaliyofanyika Pugu halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Meya Mwita alisema wakina mama ndio msingi mkubwa ndani ya familia , Taifa  kutokana na mchango ambao huutoa  jambo ambalo linaleta ustawi mkubwa maendeleo.

Aliongeza kuwa licha  ya changamoto ambazo hukutana nazo lakini wamekuwa ni watu  wasio kata tamaa hivyo akasisitiza kuwa wakina baba wanatakiwa kutoa ushirikiano wao kwa silimia 100.

Aidha Meya Mwita aliwapongeza wa kina mama kutokana na ubunifu waliokuwanao kila kukicha katika kujitafutia maendeleo na hivyo kuwa msaada mkubwa ndani ya familia zao ikiwemo kuwasaidia majukumu wakina baba.

“ Natambua mchango wenu sana, mmekuwa wabunifu , mnajishugulisha kwenye mambo mbalimbali ya kimaendeleo, mmekuwa mstari wa mbele kutengeneza miradi ambayo inasaidia kwenye familia zenu bila hata wakina baba kushiriki.

“ Hivi sasa mmeanzisha vikoba, hii yote ni katika kujituma kwenu ili muondokane na umasikini, nawapongez sana” alisema Meya Mwita.

Akizunguzungumzia changamoto zilizopo kwenye dampo, la Pugu Kinyamwezi, Meya Mwita alisema wameanza kuandaa utaratibu ambao utawasaidia kuondokana na chagamoto hizo.

Alisema suala la dampo limekuwa ni changamaoto kubwa lakini hadi kufikia Agosti mwaka huu, uratibu huo utakuwa umeshatolewa.

Akizungumzia suala la maji , alisema kuwa Kata ya Pugu imekuwa na changamoto hiyo na hivyo kuwa kero kwa wakina mama lakini kwa sasa upo mpango wa kuwawezesha kupata visima vitatu vya maji.

Alisema kwenye shuguli za maendeleo hakuna mambo ya vyama na kwamba viongozi walipo kwenye nafasi zao wanatakiwa kuwatumikia wananchi wote ili kuhakikisha kwamba wanapata maendeleo waliyoahidiwa.

 “ Kwenye maendeleo hakuna mambo ya vyama, kila mmoja anahitaji maendeleo, mambo ya vyama hivi sasa tunayaweke kando,  ili kupata muda wa kufanya kazi moja tu, yakuwatumikia wananchi ambao mmetuchagua” alisistiza.


“ Ndani ya jiji hili tunataka kuleta maendeleo, ili mwaka kesho nikija kusimama hapa yale ambayo tunayazungumzaleo, tusiyarudie tena na badala yake tuzungumze mambo mengine.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget