Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

SINGIDA UNITED YANASA SAINI YA KIUNGO WA MBEYA CITY

Na Zainab Nyamka


Kiungo mahiri wa timu ya Mbeya City Kenny  Ally amejiunga rasmi na klabu ya Singida United kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania bara kwa kandarasi ya miaka miwili.


Kenny ni miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa wakiwindwa vikali na klabu kubwa za hapa nchini Simba na Yanga kila mmoja akitaka kupata saini yake ila walikuwa wakishindwana katika dau.

Usajili huo wa Kenny kwenda  Singida United ni pigo kwa timu ya Mbeya City kwani inaonekana ikiendelea kuvunjwa  kwa kusajiliwa wachezaji wao na klabu mbalimbali.

Singida United ni miongoni mwa timu ambazo zimeanza kutazamwa na wadau wa soka kwamamba huenda wakaleta mapinduzi katika soka hapa nchini hii inatokana na mipango yao ikiwemo usajili wa wachezaji wa kigeni.

 Mchezaji Kenny Ally akipokea jezi yake kutoka kwa Katibu Mkuu wa Singida United Abdulrahman Sima baada ya kukamilisha kutia saini kandarasi ya miaka miwili ya kuitumikia klabu hiyo, katikati ni  Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Singida Festo Sanga.

 Mchezaji Kenny Ally akitia saini kandarasi ya miaka miwili ya kuitumikia klabu hiyo. Kulia ni  Katibu Mkuu wa Singida United Abdulrahman Sima na  Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Singida Festo Sanga.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget