Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

ROONEY YUPO BONGO… UKITAKA KUMUONA BUKU 3

Wayne Rooney.

STAA wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney ambaye ametua nchini leo Jumatano na kikosi cha timu yake mpya ya Everton tayari kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia kesho Alhamisi.

Wakati Rooney akitua nchini, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limemteua mwamuzi wa kimataifa wa Tanzania mwenye beji ya Fifa, Israel Mujuni Nkongo, kuchezesha mechi hiyo ya Everton na Gor Mahia.

Rooney na wachezaji wengine wa Everton pamoja na benchi la ufundi, wametua nchini leo Jumatano kwa ajili ya kuwapa burudani Watanzania kesho Alhamisi.

Mechi hiyo iliyoandaliwa na Kampuni ya Michezo ya Kubashiri ya SportPesa, inatarajiwa kupigwa kesho Alhamisi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas, amesema mbali na Nkongo kuwa mwamuzi wa kati, wasaidizi wake watakuwa ni Ferdinand Chacha na Frank Komba. Elly Sasii atakuwa mwamuzi wa akiba, huku Michael Wambura akiwa kamishna wa mchezo huo.

Kuelekea mchezo huo, Mkurugenzi wa Utawala na Uendeshaji wa SportPesa Tanzania, Abbas Tarimba, amesema: “Maandalizi yanakwenda vizuri, Gor Mahia wamekuja leo (jana Jumanne) mchana, wakati kesho (leo Jumatano) asubuhi, tunatarajia kuwapokea Everton.”
Katika mchezo huo ambao viingilio vitakuwa ni Sh 3,000 na 8,000, mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget