Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

WAFANYAKAZI WA MV LIEMBA WATAKIWA KUWAJIBIKA

1
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akipata chakula na manahodha na mabaharia wa meli ya MV Liemba inayofanya safari katika Ziwa Tanganyika.
2
Muonekano wa meli kongwe ya MV. Liemba ikiwa imetia nanga katika bandari ya Kigoma, meli hiyo imeatkiwa kuongeza safari zake kutoka awamu tatu hadi kumi kwa mwezi.
…………………………………………………………………..
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, amewataka manahodha na mabaharia wa meli ya MV. Liemba kufanyakazi kwa ubunifu na uadilifu ili kuiwezesha meli hiyo kujiendesha kibiashara.
Akizungumza na wafanyakazi wa meli hiyo Prof. Mbarawa, ameelezea kuridhishwa na mabadiliko yanayoendelea katika meli hiyo na kuwataka wasibweteke bali waongeze ubunifu.
“Hakikisheni mnatoa huduma bora kwa wateja wenu na kupata faida ili serikali na wadau wengine wawaamini na kutumia huduma yenu”, amesisitiza Prof. Mbarawa.
Waziri Prof. Mbarawa ameitaka meli hiyo kuongeza safari zake kutoka awamu tatu hadi kumi kwa mwezi ili kuhuisha huduma za usafiri na uchukuzi katika Ziwa Tanganyika.  
Prof. Mbarawa ambaye yuko katika ziara ya ukaguzi wa miundombinu mkoani Kigoma amepata fursa ya kukagua utendaji wa meli ya MV. Liemba, kupata chakula cha pamoja na wafanyakazi wake katika meli hiyo na hatimae kutoa maelekezo kwa manahodha na mabaharia wa meli hiyo kongwe hapa nchini.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget