Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

SERIKALI YAWATAKA MA-DC NA MA-DED KUSIMAMIA MIPANGO YA MAENDELEO.

picha (1)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wakurungenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa wakati wa kufunga  mafunzo ,ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa Serikali yanayotolewa na Taasisi ya Uongozi na Ofisi ya Rais Tamisemi.
picha (2)
Baadhi ya Wakurungenzi wa Halmashauri za Mikoa sita ya kanda ya ziwa wakishiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi yaliyotolewa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tamisemi.
picha (3)
picha (4) picha (9)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo.
…………………………………………………………………………………….
Serikali imewaagiza Wakuu wa wilaya na Wakurugenzi wa halmashauri nchini kwenda kusimamia mipango ya maendeleo baada ya kupitishwa kwa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018.
 Hayo yalisemwa leo na Naibu waziri wa nchi, Ofisi ya Rais. Tamisemi Selemani Jafo kwa niaba ya Waziri mkuu Kassim Majaliwa katika kufunga semina ya siku tano kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri mjini Dodoma.
 Semina hiyo ya uongozi imelenga kuwajengea uwezo viongozi hao ili waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo na imetolewa na wataalam wa Taasisi ya Uongozi ikishirikiana na ofisi ya Rais Tamisemi.  
 Mafunzo hayo ni ya awamu ya pili na yamejumuisha viongozi hao kutoka mikoa ya Mwanza, Mara, Manyara, Kagera, Simiyu na Shinyanga huku awamu ya kwanza yalihusisha mikoa ya Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Katavi na Kigoma.
 Akifunga mafunzo hayo, Jafo amesema inatarajiwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri zote watapata mafuzo hayo kwa awamu kabla ya mwezi Septemba mwaka huu.
Amewataka kuweka mipango kazi kwa kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015.
Jafo amesema katika kusimamia mipango hiyo wahakikishe wanatoa kipaumbele katika kusimamia sekta muhimu ambazo zinagusa jamii kama Afya, Elimu na Maji.
“Jiepusheni na uzalishaji wa madeni,hakikisheni malipo hewa, safari hewa, watumishi hewa hawatokei katika maeneo yenu mnayosimamia,”amesema Jafo
Aidha, Jafo amewatahadhari kujiepusha na watu wanaofanya vitendo vya utapeli kwa kutumia majina na picha za viongozi wa juu ikiwemo Mawaziri ili kujipatia fedha.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Uongozi,Denis Rweyemamu,amesema mafunzo yanalenga kuwajengea uwezo ili waweze kufanya kazi kwa weledi.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget