Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

TANZIA ; KIFO CHA SETH KATENDE

Kwa majonzi makubwa, uongozi na wafanyakazi wote wa Efm radio na tv-E , unasikitika kutangaza kifo cha mfanyakazi mwenzetu Seth Katende – maarufu kama bikira wa kisukuma kilichotokea Julai 9 katika hospitali ya taifa Muhimbili.


Ni vigumu sana kuamini na kukubali msiba huu mzito kwetu lakini kwakuwa sisi ni binadamu na kila nafsi lazima ionje umauti, tunamuomba mwenyezi mungu aipumzishe roho ya marehemu mpendwa wetu seth katende mahali pema, Amina.


Uongozi na wafanyakazi wa Efm radio na tv-E unatoa pole kwa familia ya marehemu na wasikilizaji wetu wote walioguswa na msiba huu.


Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe, Amina.

 Marehemu Seth Katende (Bikira wa Kisukuma) enzi za uhai wake akiwa  studio, Efm redio.

Kutoka kushoto marehemu Seth Katende akiwa na timu nzima ya kipindi cha ubaoni alichokua akitangaza.

Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget