Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

The Desk & Chair Foundation yatoa msaada kwa mtoto Mlemavu


Familia ya mtoto Malale Mihayo (12) yenye makazi yake katika Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imeishukuru Taasisi ya The Desk & Chair Foundation (TD&CF) Tawi la Tanzania kwa msaada wa baiskeli (Wheel Chair ) kwa ajili ya mtoto wao mwenye tatizo la Cerebral Polse (mtindio wa ubongo).


Akizungumza na mtandao huu baada ya kukabidhiwa baiskeli hiyo mama mzazi wa mtoto huyo Elizabert Tungu alisema  itampunguzia adha ya kumbeba mwanaye huyo ambaye hana uwezo wa kufanya chochote kutokana na tatizo alilonalo.


“ Mwanangu alizaliwa  mwaka 2008 akiwa mzima wa afya, alipata tatizo hili baadaye akiwa na umri  wa miaka 3 na nusu.Nilimpeleka kutibiwa hospitali huko Arusha na Moshi madaktari wakanieleza anasumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo, licha ya kutibiwa hakupata nafuu.Nawashukuru Desk & Chair kwa msaada huu,”alisema.


Bi. Tungu mwenye familia ya watoto sita alisema alimpeleka kwa waganga wa tiba za jadi nako hakupata nafuu na hivyo akalazimika kurejea nyumbani ambapo mwanaye huyo aliendelea kukakamaa viungo vya mwili wake na kupoteza uwezo wa kukaa wala kutembea.

  Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foundation Tawi la Tanzania Sibtain Meghjee kulia, akimkabidhi Elizabert Tungu baiskeli (Wheel chair) kwa ajili ya  mwanaye Malale Mihayo (aliyekaa) ambaye ana tatizo la mtindio wa ubongo.Kushoto ni Abass Meghjee mmoja wa wafadhili na kiongozi wa taasisi hiyo yenye makao makuu nchini Uingereza.

 Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foudation Tawi la Tanzania Sibtain Meghjee akimsaidia kumsukuma Malale Mihayo mkazi wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga baada ya kumkabidhi msaada wa baiskeli (Wheel chair) itakayomsaidia kwa usafiri. Mtoto huyo ana tatizo la mtindio wa ubongo.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget