Kitaifa, Kimataifa, Siasa, Michezo na Burudani

HATIMAYE YANGA YAMTAMBULISHA AJIB NA KUMPA JEZI NAMBA 10.


Ibrahim Ajib ametambulishwa rasmi na klabu ya Yanga baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo kwenye mashindano mbalimbali kuanzia msimu wa 2017-2018.
Katibu Mkuu wa Yanga Charles Bonifasi Mkwasa na meneja wa timu Saleh Hafidh wamemtambulisha Ajib mbele ya waandishi wa habari ndani ya makao makuu ya Yanga mtaa wa Jangwani.

Awali zilianza kama tetesi huku Ajib na Yanga wote wakikanusha tetesi ambazo zilikua zikiibuliwa kwamba Ajib amesaini mkataba na Yanga.
Ajib amekabidhiwa jezi namba 10 ambayo ilikuwa inavaliwa na Matheo Anthony, Ajib ameondoka Simba akiwa anavaa jezi namba 23 ambapo kwa upande wa Yanga jezi hiyo inavaliwa na nahodha Nadir Harou ‘Cannavaro’.
Labels:

Post a Comment

[facebook]

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget